Baadhi ya wateja wa bank ya NMB  tawi la Songea wakiwa katika mstari mrefu wakisubiri kupata huduma za kifedha katika bank hiyo kama walivyokutwa na mpiga picha wetu Muhidin Amri mjini Songea leo. Inasemekana hali kama hii inaonekana karibu katika kila tawi la NMB nchini kutokana na kutumiwa na wananchi wa kipato cha kati na cha chini pamoja na wanafunzi. Rai imetolewa kwa uongozi wa benki hiyo kutafuta  njia ya kuboresha huduma zao na kupunguza adha kama hii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Jamani .. Mdau uliyeweka hii picha na ujumbe hapo chini tunashukuru sana kwani inaweza kusaidia kuodokana na tatizo hili sugu la NMB na wadau wake. Ila naomba nikuweke wazi kwamba watumiaji wa NMB sio watu tu wa kipato cha chini na kati.. hivyo U cannot generalize .. bali ni watumishi kabiribia wote wa serikali , ikiwemo na Jeshi vilevile ..sasa sijui hawa ni wananchi wa kipato cha chini??? Angalia usije chafua hali ya hewa hapa...

    ReplyDelete
  2. Mh hii sio kweli kwa sasa labda kama una lako jambo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...