Dj Emani Kwasa akiwa na mtangazaji Bony Zacharia wa radio Ebony FM  jukwaani
  

Na  Francis  Godwin
Matamasha ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika maarufu kwa jina la Mtikisiko na Voda Com na Pepsi yanayoendelea katika mikoa ya nyanda za juu kusini kwa maana ya Iringa ,Ruvuma na Mbeya yamezidi kuacha historia iliyofichika katika mikoa hiyo kwa wapenda burudani.
 
Mr Blue
Matamasha haya ya miaka 50 ya uhuru Mtikisiko na Voda Com na Pepsi ambayo tayari yamepata kuacha simulizi katika mji wa Ilula wilaya ya Kilolo na mji wa Mafinga wilaya ya Mufindi hivi sasa mashambulizi zaidi yanaelekea katika mji wa Makambako wilaya ya Njombe mkoa mpya wa Njombe ambako burudani itawashukia wakazi wa Makambako siku ya jumamosi kwenye viwanja vya Amani na jumapili wakazi wa mji wa Songea kutekwa ndani ya uwanja wa Maji maji .

Mr Blue
Katika mji wa Mafinga mashabiki wa burudani waliopata kukutana uso kwa uso na wasanii Ally Kiba ,MR.Bluu na wasanii maarufu kutoka mkoa wa Iringa Nemo pamoja na Awilo kutoka mkoa wa Mbeya ,wamepata kukishukuru kituo cha radio Ebony Fm kwa kuonyesha njia katika burudani mikoa ya nyanda za juu kusini na kuwa matamasha kama hayo hayajapata kutokea na kuomba yazidi kuendela zaidi na zaidi.
Mwenyekiti wa watuma salamu mkoa wa Iringa Dkt Said Utenga aliwashukuru waandaaji wa matamasha hayo ya miaka 50 ya uhuru Mtikisiko kilaru laru na Voda Com 2011 alisema kuwa hatua hiyo ni kubwa na inapaswa kupongezwa na wananchi na viongozi pia wa mikoa husika.
Mratibu wa Tamasha
Kwani alisema kuwa vipo vitu vingi vya radio ila kazi inayofanywa na radio Ebony Fm katika kuenzi miaka 50 ya uhuru kwa kuwakutanisha wananchi katika burudani ya pamoja ni jambo jema ambalo linapaswa kuungwa mkono.
Ally Kiba
Hata hivyo pamoja na mkusanyiko mkubwa wa wapenda burudani kujitokeza katika uwanja wa RMA Mafinga kupata burudani halisi bado umati mkubwa zaidi ulipata kujitokeza katika ukumbi wa Ebony Shimoni mafinga ambako hadi majira ya saa 8 usiku nusu ya wapenda burudani walikuwa katika foleni nje ya ukumbi wakitaka kuingia katika ukumbi huo ambao hata hivyo ulionekana kujaza zaidi kabla ya vyombo vya usalama kuwazuia kuendelea kuingia ndani ya ukumbi huo .
Kazi nzuri iliyofanywa na askari polisi chini ya afande Ghatto Mfaume na mkuu wa polisi wilaya ya Mufindi (OCD) Kakamba ya kuzuia mashabiki hao kuendelea kuingia katika ukumbi huo iliweza kusaidia kuondoa lawama kwa mashabiki hao ambao waliona kama waandaaji wa tamasha hilo na kuwa kama wanawanyima kuungana na wenzao ndani ya ukumbi kupata burudani zaidi.
Awilo wa Mbeya
Tayari mratibu wa tamasha hilo Bony Zacharia amepata kuwashukuru wadau wa burudani mjini Mafinga kwa kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo na kuwaomba radhi wale ambao walishindwa kuingia ukumbini kutokana na ukumbi kujaa zaidi.
Huku akiwataka wakazi wa mji wa Makambako ,Njombe ,Songea na Chimala na Mbeya kujindaa kwa burudani kama hiyo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...