1. Katika Globu ya Jamii, hakuna habari ama picha inayowekwa kapuni baada ya kuonekana ukurasa wa kwanza, bali  inahamia  tu ukurasa wa pili ama wa tatu ama wa nne  na kuendelea kutokana na wingi wa habari na picha zinazomiminika  kwa siku. Kwa kweli habari na picha ni nyingi kiasi kasi yake ni kali...

2. Ukitaka kuingia ukurasa unaofuata nenda chini kabisa kulia bofya penye 'Habari Zilizopita' utakuwa umepatia kupata ukurasa unaofuata. Fanya hivyo tena na tena kila ukurasa unapofunguka, nawe hutopitwa na kitu kamwe!

3. Vile vile,  ili kutafuta habari kwa jina la mtu, sehemu, ama tukio angalia juu kulia na juu ya picha ya Ankal utakuta maneno 'Tafuta chochote hapa' ndani ya kisanduku. Weka mshale wako hapo, bofya, na  hayo maneno yatapotea kisha weka jina la mtu ama kitu ama tukio utavipata bila kelele wala mikwaruzo. Mfano ukitaka habari za Rais andika 'JK' ama 'Kikwete' kwenye hicho kisanduku, utazipata zote mpya na za awali.

4. Anza namba moja. Hapa hakuna masharti wala vigezo vya kuzingatia. Wewe ni kubofya kwa kwenda mbele na kuendelea kufaidi mambo ya Globu ya Jamii. Kumbuka kwamba habari ni nyingi, kadhalika picha ni za kumwaga. Hivyo unachoona ukurasa wa kwanza haimaanishi kuwa habari zimefutwa. Ni kwamba zimehamia tu ukurasa mwingine. Hivyo kazi kwako katika kuperuzi na kudadisi....

Libeneke Oye!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...