Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mafuta nchini (TPDC), Yona Killagane, wakati walipokutana kwa mazungumzo Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkurugenzi Masoko na Uwekezaji wa Shirika hilo, Dismas Fuko.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea Nyaraka za kujisomea kuhusu Uwekezaji kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Raymond Gondwe, wakati alipofika yeye na ujumbe wake kumtembelea Makamu wa Rais kwa mazungumzo ofisini kwa Makamu, Ikulu Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) wakati walipofika ofisini kwake jijini Ikulu Dar es Salaam leo. Picha na muhidin Sufiani-OMR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...