Wazabuni wanaowania kujenga Daraja la Kigamboni  leo wamekutana katika kikao maalum kuangalia michoro ya daraja iliyochorwa na msanifu wa kazi hiyo kutoka nchini Misri.

Wazabuni hao ni kutoka makampuni 7 ya kimataifa ambayo yameteuliwa kuingia mchakato rasmi wa kondrasi ya kujenga daraja hilo.

Msanifu huyo Bw. Mohamed Shohayeb (pichani) kutoka Arab Consulting Engineers aliwaonyesha Wazabuni hao michoro ya jinsi daraja litakavyokuwa. Shughuli hiyo ilikuwa chini ya Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa NSSF Bw. Yacoub Kidula na ilihusisha watalaam kutoka NSSF na Serikalini.

Baada ya zoezi hilo, Wazabuni walipelekwa kwenye eneo litakapojengwa daraja hilo huko Kigamboni kujionea wenyewe hali halisi. Kilifuata kipindi cha maswali na majibu ambapo Wazabuni waliuliza Msanifu maswali ili kupata ufahamu zaidi wa kazi hiyo kabla ya kurudi makwao na kuwasilisha gharama zao za ujenzi.

Tarehe ya mwisho ya kuleta maombi ya kazi hiyo ni 15 Desemba 2011 ambapo maombi hayo yatafunguliwa hadhrani na mshindi atakaejenga daraja hilo kutangazwa rasmi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...