Ankali habari ya kazi,naomba niwakumbushe wadau wa Blog yetu jinsi Tanzania ilivyofikisha miaka hamsini ya Uhuru huku ikiwa na kumbukumbu adimu ambazo watu hawazijui, picha hii ilipigwa Siku ya Ijumaa Tarehe 19 October 2001 na hili ni Daraja la Mto Malagarasi kule Kigoma,nasikia Daraja hili lilijengwa long time lakini bado liko Imara kama limejengwa juzi tu,Ukitoka Kibondo lazima uvuke hapa kabla hujafika Kasulu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Reminds me of Bulumbora JKT :)

    ReplyDelete
  2. Sidhani kama magari yanaweza kupishana hapo. Inabidi yasubiriane. Sasa sijui nani anayeamua gari lipi lianze kupita kabla ya lingine

    ReplyDelete
  3. Anonymous wa Wed Dec 28, 12:44:00 AM, nadhani sheria zetu za nchi huwa zinazuia magari kuoishana kwenye daraja (sijui kwanini lakini fuatilia) pia unapokaribia madaraja ya mito mikubwa huwa kuna sign za kuonyesha kwamba mbele kuna daraja pia kuna vituta vidogovidogo. Hivyo basi mara nyingi yule anaekaribia ndio huwa anaruhusiwa pamoja na msafara wa magari yaliyo nyuma mpaka yaishe ndio na mwingine anafuatia pamoja na magari mengine.

    ReplyDelete
  4. Aah ah, usishangae: TULITHUBUTU, TULIWEZA, TUNASHINDWA NA TUNAENDELEA KUSONGA MBELE"

    Ya siku hizi hayadumu kwa ajili ya slogani hiyo hapo juu. Kuchakachua kwingi.

    Juzi juzi Mh. Magufuni alikuwa anatoa tahadhari kwani anajua.....

    Asante kwa picha mdau.

    ReplyDelete
  5. ahsante kwa picha ya kwetu!!!! Hilo daraja means a lot kwangu!!!

    ReplyDelete
  6. Hivi unadhani common sense ndiyo itamuongoza dereva mmoja amsubirie mwenzake?

    Siku moja tulikuwa darajani pale Ruvu (lile daraja la zamani). Mwenye basi letu alianza kuingia kwenye daraja na alishavuka karibu robo tatu ya daraja. Tulitegemea dereva aliyekuwepo upande wa pili asubiri kwa muda mfupi tu ili tumalizie na yeye aendelee. Cha mshangao aliingia na kutuzibia njia kabisa na akakataa kurudi. Tulikaa hapo mpaka tukamsihi yule dereva wetu awe muungwana arudi nyuma ampishe.

    Bahati nzuri yule dereva wetu alisikia na kurudi nyuma pole pole, tukampisha yule mbishi avuke.

    Kwa hivyo siyo wote wenye akili hizo unazofikiria wewe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...