Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA,Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wahitimu wa Mahafali ya Saba ya Chuo hicho (hawapo pichani) kabla ya kuwatunuku shahada zao katika mahafali hayo yaliyofanyika leo Viwanja vya Chuoni hapo Vuga Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mkuu wa Chuo kikuu cha Taifa SUZA Dk Ali Mohamed Shein,akimtunuku Shahada ya heshima ya chuo kikuu cha Taifa cha SUZA Rais Mstaafu wa Zanzibar Dr Amani Abeid Karume,wakati wa mahafali ya 7 yaliyofanyika katika viwanja vya chuo Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mkuu wa Chuo kikuu cha Taifa SUZA Dk Ali Mohamed Shein,akimkabidhi zawadi Said Salim Bakhresa,kwa mchango wakemkubwa kukisaidia Chuo,wakati wa mahafali ya 7 yaliyofanyika katika viwanja vya chuo Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha SUZA,Simai Mohamed (kushoto)na Mfanya biashara maarufu Said Bakhresa na Dr Nariman Jidawi,walipompongeza kwa kupata zawadi kutokana na mchango wake mkubwa kwa SUZA,wakati wa mahafali ya 7 chuoni hapo.
Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA wakisubiri kutunukiwa Shahada zao na Mkuu wa Chuo hicho ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika Mahafali ya Saba ya Chuo hicho yaliyofanyika leo Viwanja vya Chuoni hapo Vuga Mjini Zanzibar.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein wa katikati waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa SUZA pamoja na wahitimu wa Chuo ngazi ya Stashahada baada ya kuwatunuku Stashahada zao katika Mahafali ya Saba ya Chuo hicho yaliyofanyika leo Viwanja vya Chuoni hapo Vuga Mjini Zanzibar.picha na Ramadhan Othman IKULU ZANZIBAR.


Na Hamad Hija,
 Maelezo zanzibar
Mkuu wa chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar Suza  Dk Ali Mohd Sheni leo amewatunuku Marais wastaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya  Zanzibar wa awamu ya tano na ya  sita Shahada ya heshima ya udakitari  kutokana na mchango wao  mkubwa walioutowa kwa  masuala  mbali mbali  ya maendeleo hapa Zanzibar

Waliotunukiwa shahada  hizo ni Rais mstaafu wa awamu ya tano  Dk Salmin Amuor Juma Rais mstaafu wa awamu ya sita Dk Aman Abeid Karume ambapo shughuli hiyo ilifanyika katika viwanja vya kampasi ya chuo kikuu cha Vuga mjini Zanzibar  shugghuli hiyo ya kutunuku shahada hizo ilienda na mafahali ya saba ya chuo hichosamba mba

DkSalmin Amuor Juma  ambaye alitukukiwa  shahada hiyo ya udakitari wa heshima bila kuwepo katika tukio hilo ambalo lilifanyika leo samba mba na utowaji mwengine wav yeti na shahada mbali mbali kwa wahitimu mbali mbali wa fani mbali katika mahafali ya saba ya chuo hicho

Mbali na kazi hiyo ya kutunuku shahada hizo kwa viongozi wastaafu walioitumikia nchi yetu kwa mafanikio makubwa pia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi DkAli Mohd Sheni alikabidhi vyeti ,Stashahada na shahada kwa wanafunzi 327 wa fani mbali mbali ambao wamehitimu chuoni hapo

Kwa upande wa  wa hitimu  hao waliotunukiwa shahada ya kwanza ya sayansi na elimu walikuwa wahitimu 63 ambapo kwa upande wa wahitimu katika fani ya Diploma ya sanaa na elimu walikuwa wahitimu wapatao82

Aidha Mkuu wa chuo hicho cha Suza na Rais wa Zanzibar katika mahafali hayo ya saba ya chuo hicho Rais aliwatunuku  shahada ya kwanza ya sayansi na computer   wahitimu 11 wakati wahitimu 14 wa fani ya komputer walItunukiwa cheti kwa kuhitimu masomo hayo.

Katika shughuli hiyo ambayo ilihudhuriwa na wananchi mbali mbali na  baadhi ya mawaziri wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ambaye pia ni mkuu wa chuo hicho cha Suza aliwatunuku  shahada ya kwanza wahitimu  139 fani ya  Elimu na sanaa ambao nao wamemaliza masomo yao

Baada ya kumaliza kazi ya kutunuku vyeti na shahada na stashahda Mkuu wa chuo hicho Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein alisema kuwa kuongezeka kwa vyuo vikuu hapa Zanzibar hiyo ndio dalili moja ya maendeleo ya nchi hii

Aidha  alisema halitakuwa jambo la ajabu kwa siku za baadaye kuongeza na chuo chengine alisema tuna fanya hivyo kwa kuwa mahitaji ya kuwa na chuo chengine yapo

Akizungumzia suala la kukikuza Kiswahili alisema zanzibar ni moja ya sehemu ambayo inasema Kiswahili sanifu lakini ameseshangazwa na tabia iliyojengekaya  kuwa katika mikutano yenyewatu kidogo wasiozungumza lugha ya  Kiswahili tunalazimika kungumza kingereza amesema kuwa katika hali kama hiyo ni vyema tukazungumza lugha yetuwenyewe  na wale ambao hawajuwi tukafikishia ujumbe tu 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. yaani chai jaba nae apata honorus

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...