HABARI ZA KUAMINIKA NA KUSIKITISHA ZILIZOIFIKIA GLOBU YA JAMII ASUBUHI HII,INAELEZA KUWA MUIGIZAJI WA SIKU NYINGI WA SANAA YA MAIGIZO,MZEE FUNDI SAID MAARUFU KWA JINA LA MZEE KIPARA (PICHANI),AMEFARIKI DUNIA MAPEMA LEO ASUBUHI.

MZEE KIPARA AMBAYE ALIKUWA AKISUMBULIWA NA MARADHI KWA KIPINDI KIREFU AMEFIKWA NA MAUTI HAYO LEO MAENEO YA KIGOGO ALIKOKUWA AKIISHI.

GLOBU YA JAMII IMEPOKEA TAARIFA HIYO KWA MASIKITIKO MAKUBWA SANA NA INATOA POLE KWA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI WA KARIBU NA WAPENZI WOTE WA SANAA YA MAIGIZO NCHINI.

TUNAMUOMBEA KWA MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI.

AMEIN.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Mzee Kipara Mungu akuweke pema peponi - Amin.

    Kwa kweli katika uhai wako umetufurahisha wengi katika maigizo yenu yaliyokuwa na busara sana na bila matusi wala aibu. Ilikuwa ni michezo kweli kweli na tukifurahia tangu enzi ya Radio mpaka televisheni.

    Unakokwenda wasalimie akina Mzee Jongo, Bi Haambiliki, Pwagu na Pwaguzi na wengine wengi waliokwisha tangulia mbele ya haki.

    ReplyDelete
  2. Inna Lillahi wa Inna Ilahi Rajiun

    ReplyDelete
  3. RIP Mzee Kipara...Tulikumisi na tutaendela kukumisi!

    ReplyDelete
  4. M/mungu ailaze roho ya mzee wetu,mahali pema peponi na awape subira wanafamilia ktk kipindi hiki kigumu,poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  5. Inasikitisha sana wazee kama hawa wanaondoka duniani wakati kizazi kilichoko na kinachofanya mambo ya maigizo hakijaweza kufanya hata moja la mafunzo kwa jamii kupitia sanaa hiyo kama wazee hawa! Tunamuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya mzee Kipara mahala pema peponi.

    ReplyDelete
  6. Wacha ajipumzikie mzee wa watu

    ReplyDelete
  7. michuzi wewe ni mwandishi mzuri sana wa habari sio kama globalpublisher asubuhi wametoa picha ya kipara amekufa ukiwa wazi kabisa bila ya kufunikwa baada ya kupata malalamiko ya watu wametoa huyo sio uhandishi wa habari sio vizuri kutoa picha ya mtu amekufa thanks uncle michuzi

    ReplyDelete
  8. inna lillah waina illaih ajiun kwake tumetoka na kwake tutarejea

    m.mungu akupe malazi mema peponi ameen

    mchango wako katika kuchangamsha jamii tutaukumbuka.

    ReplyDelete
  9. Inna-Lillah_Waina -Ilaihi -Rajiun Mwenyezi Mingu amsamehe makosa yake

    ReplyDelete
  10. Hawa kweli ndio walikuwa wakiijua sanaa, na sijui ni vipi tunawaenzi watu muhimu kama hawa?
    Wenzetu ulaya watu kama hawa huenziwa daima, jamani tufanye hivyo pia.
    MUNGU ALIWEKE ROHO YAKE PEMA PEPONI, AMEN.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...