JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII




TAARIFA KWA UMMA

MSIMAMO WA WIZARA KUHUSU UGAWAJI WA

VITALU VYA UWINDAJI‏

UGAWAJI WA VITALU HAUTARUDIWA

Wizara ya Maliasili na Utalii haina mpango wa kurudia ugawaji wa vitalu. Mchakato wa ugawaji ulikamilika mwezi Septemba mwaka jana (2011) na matokeo yake kutangazwa wazi.

Mapema mwezi Septemba 2011, Wizara ilitoa orodha ya kampuni 60 zilizofanikiwa kugawiwa vitalu. Kati ya kampuni hizo, kampuni 51 ni za kizalendo na kampuni 9 za kigeni kwa kuzingatia kifungu 39(3)(b) cha sheria ya wanyamapori Na. 5, ya 2009.

Hata hivyo, kumekuwa na taarifa mbalimbali zilizoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuhusu kuwepo kwa harakati zinazofanywa na waombaji waliokosa vitalu zikihusisha kuchafuana baina ya kampuni zilizopata na zilizokosa kwa nia ya kuzorotesha sekta ya uwindaji wa kitalii kwa ujumla. Vyombo hivyo vimeripoti kuwa mchakato wa ugawaji wa vitalu utarudiwa.

Wizara inasisitiza kuwa mchakato wa ugawaji wa vitalu hautarudiwa na watanzania wanahakikishiwa kuwa hatua zilizochukuliwa na serikali za kuleta mabadiliko kwenye sekta hii tangu mwaka 2008, zimesaidia sana kuimarisha usimamizi wa Sekta hii.

Kuna mabadiliko zaidi ya 21 yaliyofanyika tangu wakati huo kwa kuzingatia Sheria ya Wanyamapori, hivyo kufanya isiwe rahisi kwa mtu au kikundi cha watu kufanya tofauti (yaani, the dicretionary powers of decision makers have been seriously controlled).

Aidha, Wizara imesikitishwa na taarifa zilizoripotiwa na gazeti moja la kila siku toleo la tarehe 10/1/2011 likinukuu taarifa kutoka Dallas, Marekani kwamba zoezi la ugawaji vitalu litarudiwa kwa shinikizo la Ikulu.

Madai hayo siyo kweli na kwamba Wizara haijapokea maelekezo yoyote kutoka Ikulu wala sehemu nyingine yoyote kuhusiana na suala hili la vitalu.

Wizara inasisitiza kuwa waombaji waliopata vitalu wamehakikiwa na Waziri na kuwa barua walizopokea kutoka Wizarani kuhusu kugawiwa vitalu ni nyaraka halali za Wizara.


BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...