UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
DAR ES SALAAM UNIVERSITY STUDENTS
ORGANISATION (DARUSO)
P. O. BOX 35080-DAR ES SALAAM-TANZANIA

TAARIFA KWA UMMA.
Kikao cha Baraza la Chuo kilifanyika tarehe 10/01/2012 na kujadili hali ya Chuo kwa ujumla na

Serikali ya DARUSO iliwakilishwa. Hivyo basi Serikali ya Wanafunzi inapenda kuutaarifu umma yafuatayo:

1. Serikali ya wanafunzi (DARUSO) haijafutwa, ipo na inaendelea kufanya kazi. Kuhusu taarifa zilizoenea katika vyombo vya habari kuwa DARUSO imefutwa ni uzushi na tunafanya taratibu za kuwachukulia hatua watu na vyombo vyote vya habari Vilivyoeneza uvumi huo.

2. Serikali ya wanafunzi inaendeleza juhudi za majadiliano kuhusu hatma ya wanafunzi ambao wamefukuzwa na kusimamishwa masomo.

3. Aidha, tunaomba wale wanafunzi wachache ambao wanaendeleza mgomo warudi madarasani na kuendelea na masomo kama kawaida. Pia serikali ya wanafunzi inasisitiza kuwa mgomo unaoendelea sio halali kwani taratibu zote za kisheria na kanuni hazikufuatwa. Kwahivyo tunawaomba wanafunzi wasitishe maandamano hayo ili kuruhusu jitihada zinazochukuliwa na viongozi wao kuzaa matunda ndani ya siku chache

kuanzia leo hii tarehe 11/01/2012.

Imetolewa na:

Hassan Mustapha

Waziri Mkuu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Hili ndilo la manufaa.

    Vijana someni wacheni migomo mutakuja kujutia muda muliopoteza baadae.

    ReplyDelete
  2. Aise poleni sana nyie vijana.Matatizo mengi ya hapo yalianza tu baada ya kile kinachoitwa COST SHARING(Kipindi cha Mutungirehi!-hivi yuko wapi huyu mtu??tulimbeba 'ju kwa ju' pale Nkrumah 1994 ilikuwa noma).Hao wanafunzi warudishwe mara moja bila Masharti..Ebu fanyeni utaratibu PUNCH irudi bwana...chuo hakichangamki bila MZEE PUNCH kurudi.

    David V

    ReplyDelete
  3. hivi tuna mawaziri wakuu wangapi jamani ifikie mahali hivi vyeo viwe na maana. Mara rais mara waziri mkuu, na Mh. Pinda nae ni nani, vipi kama wakakutana katika hafla moja nani atakuwa nani hapo. Hii ni sawa na kuwavisha majoho chekechea

    ReplyDelete
  4. we unaesema masuala ya vyeo hujaenda shule nn?maana hapo wamesema ni serikali ya wanafunzi.sasa huyo pinda wako ni wa serikali ya jamuhuri.
    comment vitu vevye akili kidogo.

    David muni
    man

    ReplyDelete
  5. Wewe waziri mkuu wa CKD una matatizo, watu wanatafuta haki yao halafu unasema eti mgomo siyo halali. Wewe umetumwa na baba yako Mkandala.

    ReplyDelete
  6. Kwanza tazameni huyo anonymous wa pili kutoka juu, aliyejiita David V. Amesema kwamba yeye ni muhitimu wa UDSM.

    Amesema kwamba matatizo yamesababishwa na COST SHARING. Lakini hawezi kueleza matatizo yapi na hiyo COST SHARING imesababishaje matatizo hayo.
    Na jee, wakati wa utawala wa Nyerere ambapo hapakuwa na hiyo COST SHARING chuoni hapakuwa na matatizo haya?


    Kisha anatoa amri kwamba hao wanafunzi warudishwe mara moja bila masharti.

    Baadaye anasema fanyeni PUNCH irudi. Bila ya mzee PUNCH chuo hakichangamki. Wakati wote tunaelewa kwamba PUNCH ilikuwa ni "criminal organisation". Msomi huyu anasema kwamba pasipo crimes chuoni, basi chuo hakichangamki.

    Msomi wetu huyo. Na tena kama alikuwa UDSM mwaka 1994, maana yake ni kwamba huyu sasa ni mtu mzima kabisa. Lakini akili zake ndiyo hivyo tena, zimeelekea kusini.

    ReplyDelete
  7. Tatizo kubwa katika hiyo COST SHARING ya sasa wanaopata kipaumbele kikubwa ni wale ambao wazazi wao wanazo ambao HAWASTAHILI KABISA!

    ReplyDelete
  8. Wewe bwana titus said unakosoa bwana david. Mbona wewe hutoi msimamo wako? Wewe unataka nini.

    My take: Chuo kimebadilishwa kuwa uwanja wa siasa, maana huwezi kufukuza wanachuo halafu unasema wasiruhusiwe kujiunga na chuo chochote cha umma maana huu ni uhuni.

    ReplyDelete
  9. Wewe bwana titus said unakosoa bwana david. Mbona wewe hutoi msimamo wako? Wewe unataka nini.

    My take: Chuo kimebadilishwa kuwa uwanja wa siasa, maana huwezi kufukuza wanachuo halafu unasema wasiruhusiwe kujiunga na chuo chochote cha umma maana huu ni uhuni.

    ReplyDelete
  10. Wewe bwana titus said unakosoa bwana david. Mbona wewe hutoi msimamo wako? Wewe unataka nini.

    My take: Chuo kimebadilishwa kuwa uwanja wa siasa, maana huwezi kufukuza wanachuo halafu unasema wasiruhusiwe kujiunga na chuo chochote cha umma maana huu ni uhuni.

    ReplyDelete
  11. watanzania tumezaliwa na kulelewa katika mazingira yanayotufanya wajinga wa kudai na kutaka haki zetu. wengine hamjui wanafunzi wanachodai alafu unasema wanatumwa, mara siasa. we ndo mjinga. kama hujui kudai haki yako, waache waume zako wakutafutie haki zako. FREEDOM IS NOT FREE''

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...