Naibu Waziri wa Uchukuzi 
Athumani Mfutakamba
Naibu Waziri wa Uchukuzi Athumani Mfutakamba amesema usafiri wa reli ya kati uliokuwa umesitshwa kwa muda unatarajiwa kurejea tena baada ya kazi ya matengenezo ya maeneo yaliyoharibiwa na mvua katika stesheni ya Gulwe na Godegode kukamilika kwa asilimia 80.

Dk Mfutakamba alieleza hayo wakati akizungumza na uongozi wa reli ya TRL karakana ya Morogoro mara baada ya kutembelea karakana hiyo kuona shughuli mbalimbali za utengenezaji na ufufuaji wa injini za treni ukiendelea.

Dk. Athumani Mfutakamba alifanya ziara hiyo baada ya Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kufanya zoezi la kuwarejeshea nauli zao wasafiri wapatao 1920 ambao walikuwa wasafiri na treni kutoka Dar kwenda Kigoma siku za Jumamosi Jan 07, 2012 na Jumanne Jan 10, 2012 ambazo zimelazimika kufutwa baada ya reli ya kati kuharibika.

Ambapo pamoja na mambo mengine alisisistiza umuhimu wa wahandisi wa karakana hiyo ya TRL kuharakisha ufufuaji wa injini kutokana na uhitaji mkubwa uliopo wa ubebaji wa mizigo na abiria kwa gharama nafuu katika reli hiyo ya kati kwa wakazi wa mikoa ya Tabora na Mwanza.

Pia aliwataka wataalamu hao wa TRL kutumia vipuri vya ndani ya nchi kwa kushirikiana na shirika la mzinga na mang'ulaili kupunguza gharama badala ya kuagiza kutoka nje.

Kwa upande wake meneja wa karakana ya TRL Morogoro mhandisi Ngosa Ngosomwile alisema kuwa tayari serikali imeipatia kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa kupitia kampuni ya kusimamia mali za shirika la reli RAHCO kwaajili ya matengenezo ya injini 5 na kununua vipuri vya magari yanayoendelea na kazi.

Aidha ameomba vipuri vinavyoshikiliwa na RAHCO wapatiwe ili viweze kutumika katika kukarabati baadhi ya injini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. bongo kweli joto yani jamaa jasho mpaka kwenye macho

    ReplyDelete
  2. Isigekuwa kitu cah aibu kama tungewaomba Wajerumani waje watujengee tena reli kwani wenyewew tumeshindwa,duniani pote reli ndio usafiri rahisi na wa uhakika lakini toka tujengewe 1800 ad watu wameongezeka lakini sisi tumeshindwa hata kufikiria kuboresha usafiri huu.Kila serikali ni porojo tu siku zxinaenda wananchi wanaadhirika.Uingereza wabunge.malikia mawaziri wanasafiri kwa treni nanyi viongozi jaribuni muone adha wanazopata wananchi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...