Utabiri huu unaweza ukachukuliwa kama kwamba ni utabiri wa kinajimu kutabiri matukio ya baadaye.  Lakini si hivyo kamwe! Nyendo za sayari zinafahamika kwa kutumia usahihi wa kihisabati wa maelfu ya miaka ijayo. Kinachoelezwa kwenye makala haya ni matukio ya kufurahisha yanayoweza kutazamwa usiku angani katika mwaka mzima huu.  Yamebainishwa kwa kutumia programu ya kompyuta ya “Stellarium”na kukokotolewa na wataalamu wa astronomia, kwa mfano mtaaalam Fred Espanack wa NASA.
 
Utajiuliza,“Kwa nini unatolewa utabiri wa sayari tu, na siyo wa nyota?” Hofu ilikuwa kwamba ingetolewa kama utabiri wa nyota, ungeweza kuchukuliwa kama utabiri kwa njia ya unajimu au ufalaki, ambao si wa kisayansi. Kusema kweli, kutabiri mwendo wa nyota za kawaida angani si mgumu, kwa vile nafasi za mpagilio ya Makundi ya Nyota angani huwa haubadiliki.  Kinachobadilika ni kusogea kwa Makundi ya Nyota kutoka mashariki kwenda magharibi kama vile Jua linavyosogea wakati wa mchana ambayo inatokana na mzunguko wa Dunia yetu katika mhimili wake.
 
 
Nyota ziko umbali wa matrilioni ya kilomita kutoka kwetu, kwa hiyo nafazi zao zinabaki vile vile kwa maelfu ya miaka.  Ndiyo maana Makudi ya Nyota daima zina mpangilio huo huo na kupewa majina maalum kutokana na maumbo yanayo tokana na mpangilio huo.  Kwa mfano Kundi la Nyota linaloitwa Nge linaonyesha umbo kama la nge angani.  Maumbo ya Makundi ya Nyota hayajabadilika tangu uchunguzi wa kiastronomia ulipoanza maelfu ya miaka iliyopita.
 
Ukishatambua mpangilio wa Makundi ya Nyota, utaelewa upande gani  kuangalia ukitaka kuona Kundi fulani usiku.  Tahadhari kwamba Makundi ya Nyota pia yanasogea polepole kutokana na mzunguko wa Dunia kuiziunguka Jua.  Kuelewla kiasi gani nyota zitasogea kutoka na mzunguko huu huhitaji utaalamu lakini siyo sana .
 
Sayari, kwa upande mwingine, ziko umbali mdogo sana kutoka kwetu ukilinganisha na umbali wa nyota.  Sayari ziko mamilioni ya kilometa wakati nytoa ziko matrilioni ya kilometa.  Pamoja na hiyo sayari huzunguka Jua. Kwa hiyo, sayari huhama angani kwa kiasi kikubwa siku hadi siku. Kuelewa nafasi za sayari angani unahitaji utaalaamu mkubwa.
 
Tukio kubwa na muhimu zaidi la kuangalia mwaka huu ni Mpito wa Zuhura Juani mapema alfajiri tarehe 6 Juni. Hili ni tukio la kipekee katika maisha yetu kwa sababu tukio jingine kama hili halitatokea kwa zaidi ya karne moja, hadi Desemba 2117.  Jiandae kuona tukio hilo kwa kutumia miwani ya kuona kupatwa kwa jua itakyokuwezesha kuona sura ya Jua.  Asubuhi ya tarehe 6 Juni kuanzia mawio, saa 12:33 asubuhi, tutaweza kuona sayari ya Zuhura kama doa, likisogea polepole katika sura ya Jua karibu kabisa na ukingo wake ikiwa ni katika mwisho wa Mpito wa Zuhura Juani.  Katika hatua ya mwisho, itachukua kiasi cha dakika ishirini kuanzia saa 1:36 hadi saa 1:54 asubuhi kwa doa la Zuhura kuvuka ukingo wa Jua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. UCHAWIIIIIIIIIIIIIII!!!

    ReplyDelete
  2. Taarifa nzuri sana, ingefaa watoto wetu wa Sekondari na vijana wa vyuoni wawe wanasoma makala kama hizi. This is the practical experience of the solar system.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...