Balozi Maajar akimsikiliza mwalimu wa Chuo cha Milwaukee Area Technical College (MATC)  akionyesha mitambo ya kujifunzia na kuelezea jinsi wanafunzi wa chuo hicho wanavyotumia teknolojia kujifunza kwa vitendo mitaala ya ufundi wa nishati ya umeme
 Balozi Maajar akiwa kwenye studio ya radio ya WUWM (Milwaukee Public Radio) akizungumzia madhumuni ya ziara yake Jimboni Wisconsin kwenye kipindi mashuhuri cha Lake Effect kinachorushwa na mtangazaji Mitch Teich jijini Milwaukee. Listen to full Lake Effect Radio Interview at
 Balozi wa Tanzania nchini marekani Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar akipewa zawadi na Makamu wa Rais wa kampuni ya A. O. Smith Corporation Bw. Steve Rettler mara baada ya kuzungumza na wawakilishi wa makampuni takriban thelathini kutoka miji mbalimbali ya Wisconsin wenye nia ya kufanya biashara na Tanzania  
 Balozi Maajar (katikati) kwenye picha ya pamoja uongozi wa Chuo cha ufundi cha Milwaukee Area Technical College baada ya kumaliza mazungumzo ya awali kuhusu kuanzisha ushirikiano kati ya chuo hicho na mojawapo ya chuo cha ufundi cha Tanzania.  Kushoto kwa balozi ni muasisi wa ushirikiano wa miji ya Milwaukee na Morogoro, Ryan Skyfe na kulia kwa balozi ni Makamu wa Rais wa Chuo hicho Bibi Vicki Martin akifuatiwa na Rais wa Chuo hicho (mwenye tai) Bw. Michael Burke tarehe 20.02.2012.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Mwanaidi Maajar akiwa na Meya wa Mji wa Milwaukee Mhe. Tom Barrett wakionyesha bango lenye hati ya kuitambua siku ya tarehe 20.02.2012 kama siku ya Tanzania mjini Milwaukee.
Balozi Maajar akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Watazania waishio kwenye mji wa Milwaukee, Jimbo la Wisconsin waliofika hotelini kwake kumpokea mara baada ya kuwasili mjini hapo kwa ziara ya kikazi .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...