Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akiongea jambo na aliyekuwa Mwakilishi Mkuu wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania Zhao Zhongqiu leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam . Zhongqiu alimtembelea waziri huyo kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akisalimiana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania Lin Zhiyong leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam . Zhiyong anachukua nafasi ya Zhao Zhongqiu ambaye amemaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk.Mary Nagu akiongea na ujumbe wa wawakilishi wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania walipomtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam . Ujumbe huo uliongelea mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kibiashara kati ya Tanzania na China.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk.Mary Nagu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania walipomtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Lin Zhiyong ambaye ni Mwalikishi mpya na kulia ni Zhao Zhongqiu ambaye amemaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.Picha na Anna Nkinda - Maelezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...