Ankal akiwa na Wazee wa Kazi wa Serengeti Freight Forwarders Waarabu Chris na Muhisin Uwanja wa Nyumbani barabara ya Ripple Road, Barking, London, IG11 OSN ambako sio pa kukosa uwapo katika jiji hilo kwani pana machopochopo yote ya nyumbani na muziki wa home.
 Ankal akitoa zawadi kwa mshindi wa pili wa Pool wa wiki hii Uwanja wa Nyumbani. Kila Jumatno kuna mtanange wa Pool ambapo mshindi wa kwanza na wa Pili huondoka na mkwanja swaaafi
 Ankal akitoa zawadi kwa mshindi wa kwanza wa Pool wiki hii Uwanja wa Nyumbani
 Menyu ya Uwanja wa Nyumbani. Ugali, nyama choma na Kisamvu.... Acha!
 Ankal akiwa na anko Abuu, mwenyeji wako wa Uwanja wa Nyumbani
Hapo gemu la pool linataka kuanza na tayari wafadhili wameshapandisha chata yao..

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. safi sana vijana wa london, hii ndio inatakiwa sio watu kupiga domo tu mnatakiwa mnafanya mavitu kama haya, Hongera sana wazee wa kazi na abuu . BIG UP!

    ReplyDelete
  2. ankal angalia wasikulishe kiti moto!

    ReplyDelete
  3. Ankal ugali wote na nyama zote hizo utamaliza peke yako!! Lakini sawa maana huko baridi nyingi ina bidi uweke mavituz tumboni. kIla la heri mzee.

    ReplyDelete
  4. Ankal hebu acha ubahili. kwenye picha mpo watatu lakini sahani za ugali zipo mbili, nyama sahani mbili, chupa mbili,vichupa vya chumvi viwili na glasi mbili. Hivi kweli mmeshindwa kumlipia mwenzenu chakula chake mpaka ajibane kwenye sahani zenu kiasi hicho? Kwani maisha yamekuwa magumu kihivyo?

    ReplyDelete
  5. Ugali ni chakula ambacho haunilishi hata kwa dawa.

    ReplyDelete
  6. hongera kaka wa uwanja wa nyumbani, maisha ni popote alimradi huvunji sheria za nchi husika mambo mswano... ujasiriamali oyeee!

    ReplyDelete
  7. Ankal naona picha ya juu kabisa unafakamia ugali na cholesterol. Kumbe tuko wengi. Anyway, hiyo sehemu inaonekana imetulia sana. Nikija London itabidi nipatafute. Hapo panaonekana ni home away from home.

    ReplyDelete
  8. Ankal walahi mimi nipasie nyama finyango moja tu!

    ReplyDelete
  9. Kiti moto kwa UK tena si ndio kwao,,,hujui Msafiri Kafiri?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...