Ubalozi wa Tanzania  Brussels (Ubelgiji) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Watanzania, Chuo Kikuu cha Gent na sponser(VLIR) wanasikitika kutangaza kifo cha Mwanafunzi Ndugu  William Lufundisha, kilichotokea tarehe 15/02/2012 katika Chuo Kikuu cha Gent, Ubelgiji. 

Jumuiya ya Watanzania na marafiki wa marehemu Lufundisha wanafahamishwa kwamba tarehe 23/02/2012  saa 8 kamili alasiri itafanyika ibada ya kumuaga marehemu kwenye kanisa lililopo katika hospitali ya  Plafijn Ziekenhuis ( Plafijn hospital), HENRI DUNANTLAAN 5, 9000 GENT.

Ubalozi pamoja na Jumuiya ya Watanzania watafarijika na ujio wa watakaoweza  kuhudhuria ibada hii ya kumuaga mpendwa wetu Marehemu William Lufundisha.
 Mola aiweke Roho ya Marehemu mahala pema Peponi 
- Amina

Imetolewa na Ubalozi na Jumuiya ya 
Watanzania Brussels, Ubelgiji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Mpendwa, rafiki yetu sana Willy hakika umetuacha ukiwa kijana kabisa na bado tukikuhitaji katika ujenzi wa taifa letu katika fani ya uvuvi hasa ufugaji wa viumbe maji (Aquaculture).

    Mwenyezi Mungu akupe raha ya milele na upumzike kwa amani, AMINA.

    ReplyDelete
  2. Daah, imenigusa sana hii taarifa. RIP man. Uvuvi umepoteza mpiganaji...
    S. Mgeleka
    Kijitonyama, DSM.

    ReplyDelete
  3. RIP William

    ReplyDelete
  4. Gone too soon , at a very tender age.. RIP William ...RIP

    ReplyDelete
  5. Poleni sana wazazi, ndugu, marafiki na wafanyakazi wote wa wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. R.I.P William

    ReplyDelete
  6. kazi ya mungu haina makosa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...