Semina ya UNHCR - Protection Induction iliyofanyika Mpanda tarehe 25/01/2012 kwenye ukumbi wa mikutano wa Idara ya maji wilaya ya mpanda na kushirikisha Asasi za kiserikali, mashirika ya kitaifa na kimataifa na wadau mbali mbali.

Washiriki wa semina wakiwa kwenye kipindi

Mwendeshaji mkuu wa semina Wakili Godlove Kifikiro ambaye ni Protection Associate wa UNHCR field office mpanda, akiendesha semina ambapo aligusia juu ya shughuli za UNHCR, maana ya mkimbizi, haki na wajibu wa mkimbizi na sheria ya mkimbizi ya Tanzania ya mwaka 1998

Ndugu Michael Kiimbila, ambaye pia ni mshauri wa maswala ya kiusalama UNHCR Mpanda akitoa mada juu ya kusikiliza na kupeleleza matukio ya kihalifu kwenye kambi za wakimbizi


Baadhi ya washiriki wa semina wakipata msosi

Washiriki wa semina wakipata msosi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Huyo jamaa picha ya pili kutoka chini mbona ana sahani mbili za msosi? Au kuna mtu kamchukulia?

    ReplyDelete
  2. sasa wewe mdau wa hapo juu swali gani unauliza kama kajipendelea sahani mbili au kamchukulia mtu inasaidia nini?

    mwache mtu ajinafasi maisha mafupi sana angalia watoto wa kova wenyewe wanajiwahi maana ofisi zao hazina hata restaurant wenyewe wanakula kwa mama ntilie wakiwa kazini.

    ReplyDelete
  3. Hizi ndio Semina zinazo rubuni watu wetu kuendelea kukubali sera za Shirika la Wakimbizi bila kujali maslahi ya nchi yetu. Watu wetu hawana budi kuamka na kuacha kutapeliwa na watu waojali tu ajira zao. Wakimbizi warudi kwao. Nchi yetu ndio nchi pekee duniani inayotoa uraia wa halaiki kwa Wakimbizi. Wazungu hawadhubutu huko kwao lakini wanauza sera hiyo kwetu kwakutumia pesa yao na wenzetu wenye njaa.

    ReplyDelete
  4. jamaa ame-bust! nakumbuka enzi za JKT...

    sio ubishi, ame-bust. ingekuwa sivyo then tungeona chupa mbili za soda hapo pembeni, but ni moja inaonyesha share zote ni zake....

    ReplyDelete
  5. mwenye sahani ya pili kaenda kunawa mikono.

    ReplyDelete
  6. Hi hi hi hi hiiiii......Jamani jamani, kaa mnaona kweli kweli...yaani mimi nisingewaza kabisa kuwa; jamaa ana sahani 2.
    Ila inaonekana ni yakwake kabisa, maana ipo karibu sana nae. Maisha magumu Bongo, acha ale maisha mtu wa watu anapopata chanzi ndo hapo hapo.

    ReplyDelete
  7. Hapo Wabongo ndo mnapobolonga,
    yaani huyo mchangiaji wa hapo juu yeye kaona wakimbizi tu.
    mbona wazungu wanakuja wanachukuwa kila kitu hapo TZ na hamsemi kitu,,, waafrica wenzenu kuomba ukimbizi nchini kwenu ndo imekuwa nongwa.
    mkiwa mnatoa maoni fikilieni kwanza hata kama TZ hakuna vita ila watZ wanauana wenyewe,, angalia mambo mangapi yanatokea na waTz mmekaa kimya, umeme, Madini na mambo mengi kila siku mtanzania anazidi kuwa masikini kwa sababu ya uongozi mbovu.
    hicho ndo cha kuongelea na siyo ooh wakimpizi,,, nyambafu kabisa..

    ReplyDelete
  8. Annony wa Feb 04, 10:47:00 PM aonyesha kuwa ni mkimbizi! Anadai waTZ tunauana wenyewe kwa wenyewe!! Huyu kweli kasahau kilichomtoa kwao; kuuana wao kwa wao! Nakubaliana na Annony wa Feb 04, 04:39:00 PM wazungu wanaturubuni tu. Hakuna shida ya kukaa na wakimbizi tena nchi zao zone sasa kuna akheri; warudi!

    ReplyDelete
  9. Kula siyo mpaka uandikiwe na Daktari ukizingatia madaktari wenyewe wamekataa kazi. Ninyi mmeona sahani mbili na soda moja je lita 1.5 ya maji ya k'njaro hamjaiona? nahisi nyuma yake kuna CHARLES GLASS, TEHE TEHE TEHE!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...