Mhadhiri mwandamiz, Marehemu John Franklin Chekani
Familia ya marehemu John Franklin Chekani wa Mzumbe- Morogoro, wanatoa shukrani zao za dhati kwa madaktari na manesi wote wa Hospitali ya AghaKhan -Dsm Tanzania na Hospitali ya Roman Catholic ya Windhoek-Namibia, waliojaribu bila kuchoka kuokoa maisha ya mpendwa wetu.
Pia tunamshukuru Katibu Mkuu na wafanyakazi wote wa TAMISEMI, Mkurugenzi na wafanyakazi wote wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) Tanzania, Mkuu wa chuo, mlezi, wafanyakazi na wanafunzi wa chuo cha Polytechnic, Mch. Noleen West na washarika wote wa kanisa la mtakatifu George, familia za bw. Tomeka, bw. Mahindi, mwenyekiti,na wanajumuiya wote wa Tanzania wanaoishi Namibia waliojitokeza kwa moyo mmoja.
Shukrani za dhati pia ziwaendee Mrs. Jane Fatukubonye, Mariam Mbegu,na wanajamii wa Mkongeni na Mzumbe kwa juhudi za uwezeshaji wa msiba huo.
Pia tunazishukuru kwaya zote zilizoshiriki, kwaya ya mzumbe, ya Dodoma na kwaya ya kibaha na wachungaji wote walioshiriki katika msiba.Pia tunawashukuru wote ambao kwa namna moja au nyingine wamewezesha kutufariji katika kipindi hiki kigumu cha kufiwa na mume , baba na babu yetu mpendwa
Shukrani za dhati kabisa ziwaendee wote mliotufariji na kuwa nasi kwa namna mbalimbali. Ahsanteni kwa maombi yenu,faraja zenu na msaada wote wa khali na mali katika kipindi hiki kigumu.Mungu awabariki wote.
Mr John Franklin Chekani utakumbukwa sana na mke wako mpendwa Susana, vijana wako Franklin and Jumbe –Victor, binti yako Anneth, mkwe wako Catherine, mama yako mpendwa Annes Cynthia, wajukuu wako Nicole na Susana , dada zako, kaka zako na ndugu wote na marafiki.
Misa ya shukrani itafanyika nyumbani kwa marehemu tarehe 11 februari, 2012 kuanzia saa 3 kamili asubuhi. Misa hiyo itafanyika nyumbani kwa marehemu Mzumbe Morogoro. Wote mnakaribishwa.
“Naye atapangusa kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwa tena, wala maombolezo, wala kilio, wala uchungu hautakuwa tena, kwa maana maneno ya kwanza yamekwisha kupita.”
Rev. 21 vs. 4
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMINA.
Mungu ailaze roho ya marehemu CHEKANI mahali pema peponi Amen.
ReplyDeleteNaamkumbuka sana Mr.Chekani Alikua mtaalamu wa Cost Accounting!mifanino yote ya kufundishia alikua
anatoa kichwani! ama kweli Taifa limepoteza jembe!
RIP! Prof. Chekani. Sio Familia tu iliyopoteza mpendwa wao, Taifa pia limepoteza mmoja wa wataalamu wake wa ufundishaji wa maswala ya uhasibu na fedha. Mie pia nilifundishwa na Chekani somo la Cost Accounting kulikuwa hakuna mfanowe.
ReplyDeleteApumzike mahali pema mzee wetu.
ReplyDelete