Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akionyeshwa kito kinachotengeneza Lulu ambayo hufanywa Pete na Katibu wa Kampuni ya Ukweli ni Njia Safi Bi Safia Hashim alipotembelea kikundi cha akina mama cha Bweleo Wilaya ya Magharibi Unguja wakati wa Ziara yake ya kuangalia Miradi ya Maendeleo ya [TASAF] inafadhiliwa na Serikali ya Muungano.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Muugano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo kwa Bi Mwajuma Mwinyi kuhusu Matumizi ya Mwani wa Baharini ambao wanatengenezea Sabuni ya Kuogea na huweka Unyevunyevu kwenye ngozi kuifanya nyororo wakati wa Ziara yake ya kutembelea Miradi ya Maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ya Muugano huko Bweleo Wilaya ya Magharibi Mjini Unguja[Picha na Ali Meja]
======== ===== ===================== ==============
Na Ali Issa Maelezo.
Mamlaka ya kusimamia uvuvi wa bahari kuu Tanzania imeimba serikali ya jamuhuri ya muungano Tanzania na ile ya Zanzibar kuiridhia sheria ilopo na kuipitisha iliweze kufanya kazi zake vizuri na kutekeleza vyema kazi zake mamla.
Hayo yamesemwa leo huko kinazini katika jengo la ZSTC Zanzibar na Mkurugenzi wa mamlaka hiyo Geofrey Frank Nanyaro wakati wamazungumzo kati ya malaka na Ofisi inayo shughulikia masuala ya muungano Tanzania mbele ya waziri Samia Suluhu Hasani aliofika hapo akiwa ziarani kutembelea maeneo hayo .
Amesema malaka ya kusimamia bahari kuu ni taasisi ilio undwa kupitia sheria ya malaka ya kusimamia uvuvi kwenye eneo la ukanda wa kiuchumi EEZ ya mwaka 1998 ambayo ilifanyiwa marekebisho kupitia sheria namba nne ya mwaka 2009 sheria ambayo ilishirikishA Pande zote mbili za muungano na badalayake ikapelekwa baraza la mawaziri na kukubaliwa lakini upande wa pili wa baraza la wawakilishi hadisasa bado kuridhia sheria hiyo .
Amesema kuchelewa kuridhia sheria hiyo nikufanya kazi katika mazingira ambayo hayaendani na kazi kisheria na kuyafanya kuwa mazingira magumu katika utekelezaji wakazi zake kitalamu .
“Nivigumu kutekeleza kazizetu kitaalamu kwani sheria ndio inayo muongoza mtu kufanyakazi vyema hivyo ikawa sheria haijaridhiwa itakuwaje juu yakusimamia baharikuu ambao wanao kuja kuvua wanafahamu kilakitu .”alisema Geofrey . Aidha mkurugenzi huyo alisema kuwa kuchelewa kuridhiwa kwasheria hiyo kuna wakosesha frusa wataalamu wao hata kupata mafao yao kimsingi kamavile mishahara nahatimae kupata posho tu. Amesema halihiyo haipendezi kwani inaleta uchovu katka uwajibikaji na misingi boa ya kazi .
Nae mtaalamu wamtambo unao toa ripoti za meli za kigeni zinazo ingia nchini Damian Boniface Chando amesema kua Malaka hiyo hivisasa inauwezo wa kugundua meli zinazo ingia na kutoka kaita ukanda wa baharikuu zinazo vuasamaki kinyemela kwa kutumia mtambo wa Vessl monitoring system ambao wanao na unafanyakazi muda wote.
Aidha alisema kuwa mtambo huo unaweza usifanye kazi iwapo mabaharia watafanya uharamia kwa kuzima kifaa kiitwacho kwa kitaalamu transimitter na wao wasiweze kundua kama samaki wao wanavuliwa kwa kuibiwa. “Ni vizuri kujipanga kua na doria kwani mtambo huu hautoshi pekeyake iwapo mabaharia watafanya uharamia bila ya kuomba kibali na kuzima mitamboyao’alisema Boniface .
Nae waziri samia alisema wanazichukuwa changamoto zilopo na kwenda kuzifanyiakazi, lakini alisema kua wakati umefika kwa viongozi kuwa wa wazi na wakweli wanapokuwa katika vikao na kutekeleza yale wanayo yasema,Amesema katika ziara yake amejifunza mengi ambayo alikuwa hayajui na sasa anaelewa na atayapeleka munamo husika na kufanyiwa kazi.
Wazirihuyo alitembelea mamlaka ya Uvuvi wa Bahari kuu Fumba Maradi wa MACEP Bweleo kuangalia madawati yalio na TASAF skuli ya kombeni pamoja na mradi wa kinamama wakutengeneza sabuniza kuogea kwamalighafi ya mwani napete za luu kwamalighafi ya kombe za baharini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...