MAREHEMU GEORGE FREDERICK MBOWE |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Katika salamu zake hizo, Rais Kikwete amesema alimfahamu Marehemu George Mbowe enzi za uhai wake kama mchapakazi hodari aliyelitumikia Taifa lake kwa uzalendo, uaminifu na uadilifu mkubwa katika sehemu zote alizowahi kufanya kazi ikiwa ni pamoja na katika Utumishi wa Umma.
“Enzi za uhai wake, nilimfahamu Marehemu George Frederick Mbowe kama mtu aliyejituma kikamilifu katika utekelezaji wa majukumu yake na mchapakazi hodari”, amebainisha Rais Kikwete katika salamu zake. Amesema sifa hizo alizionyesha alipokuwa katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) na hata katika nyadhifa za Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Mwenyekiti wa PSRC na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).
Rais Kikwete ametoa pole nyingi kwa familia ya Marehemu George Mbowe kwa kuondokewa na mhimili muhimu wa familia, na amewahakikishia wanafamilia kwamba yuko pamoja nao katika kuomboleza msiba huu mkubwa. Amewaomba wawe na moyo wa uvumilivu na ujasiri katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo ya mpendwa wao kwani yote ni mapenzi yake Mola.
Rais Kikwete amesema anamuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipumzisha roho ya Marehemu George Frederick Mbowe mahali pema peponi, Amina.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
01 Machi, 2012
NB: Msiba upo nyumbani kwa marehemu Plot. No. 94, Msasani, Old Bagamoyo Road jijini Dar es salaam karibu na nyumbani kwa Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi.
Misa ya kumuaga marehemu itafanyika ijumaa saa nane mchane katika kanisa la Anglican St Alban. Heshima za mwisho zitatolewa pia nyumbani siku ya Ijumaa saa 12 jioni. Mazishi yatafanyika Dodoma siku ya Jumapili saa kumi jioni.
NB: Msiba upo nyumbani kwa marehemu Plot. No. 94, Msasani, Old Bagamoyo Road jijini Dar es salaam karibu na nyumbani kwa Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi.
Misa ya kumuaga marehemu itafanyika ijumaa saa nane mchane katika kanisa la Anglican St Alban. Heshima za mwisho zitatolewa pia nyumbani siku ya Ijumaa saa 12 jioni. Mazishi yatafanyika Dodoma siku ya Jumapili saa kumi jioni.
Kitu ambacho huwa sielewei ni kwani nini taarifa hizi za kiswahili zinakuwa na header paper za kiingereza? Kurugenzi ya Ikulu vipi?
ReplyDelete