Mkurugenzi wa Chuo Cha Biashara za Nje cha Nchini India (IIFT) Thomas Chako akiongea katika mahafali ya 12 ya Shahada ya Uzamili inayotolewa na chuo hicho kwa ushirikiano na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM ) cha Dar es salaam. Chako alikabidhi veti kwa wahitimu takribani 31. Wengine pichani kutoka kulia ni Makamu wakuu wa Chuo cha IFM Prof. Jairo na Prof. Tadeo Satta na Mkuu wa Chuo hicho Prof Godwin Mjema. Chako alihimiza umuhimu wa Tanzania kuzalisha wataalamu wa kutosha wa biashara za kimataifa ili kunufaika na fursa za biashara za ulimwengu.
Mathew Shayo(Kulia)akipokea cheti chake cha kuhitimu shahada ya uzamili ya usimamizi wa biashara za kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Biashara za Kimataifa cha India (IIFT) kutoka kwa Mkurugenzi wa Chuo hicho. Thomas Chako katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki Dar es Salaam. IIFT huendesha kozi hiyo ya MBA-IB kwa ushirikiano na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) cha Dar es salaam. Wanaoshuhudia ni Makamu wakuu wa Chuo cha IFM, Profesa Isaya Jairo (wa pili kulia) na Profesa Tadeo Satta. Chako alihimiza umuhimu wa Tanzania kuzalisha wataalamu wa kutosha wa biashara za kimataifa ili kunufaika na fursa za biashara za ulimwengu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera sana Mathew Shayo!!!!!

    Makongoro Wassira

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...