Sina uhakika sana ila naanza kuandika hiki kipande nikiamini kwamba unajua nini maana ya mitandao ya kijamii (social networks). Siku hizi makampuni makubwa makubwa duniani yanaajiri wataalamu wa kitu kinachoitwa New Media/Social Networks.Wengi wao ni vijana wadogo tu ambao aidha ndio wametoka vyuoni au wamejiari kwa kutumia mitandao jamii.

Leo naomba nigusie kidogo mtandao wa Twitter na kwanini nashauri ujiunge nao.Endapo unatumia e-mail hivi leo basi ni wazi kwamba kama bado hujajiunga au kufungua akaunti yako ya Twitter,basi hivi karibuni itakubidi. Mimi binafsi ni mtumiaji wa Twitter japokuwa siwezi kujiita mtumiaji mkubwa kwani bado sijafikia spidi ya kupost zaidi ya mara kumi kwa siku.Spidi zangu zinatofautiana

Sababu ya Kwanza: Ni vizuri mapema kabisa ukachukua username yako. Kila siku majina ya watu yanazidi kuchukuliwa.Hakikisha umechukua lako mapema kwani tofauti na mitandao inayotoa huduma za barua pepe(e-mail),mtandao wa twitter.com ni mmoja tu. Kwa hiyo ukikuta jina lako limechukuliwa utakuja kuishia au kupaswa kuchukua jina kama jumapachu76654256 kwa sababu tu twitter.com/jumapachu itakuwa imechukuliwa

Sababu Ya Pili: Nenda na wakati kwa kuelewa kinachoendelea katika ulimwengu wa tekinolojia ya mawasiliano.Hili ni muhimu zaidi kama una watoto au unatarajia kuwa na watoto. Mimi nina watoto.Ni muhimu kujua kinachoendelea mtandaoni kwani watoto wa siku hizi,tofauti na enzi zetu,wao ni watumiaji wazuri zaidi wa mitandao.Na huko,kwa bahati mbaya,wapo watu wasio na utu wala maadili.Usiposimamia usalama wao,utakuwa unafanya makosa kama mzazi.Chukua hatua,nenda na wakati.

Sababu Ya Tatu: Ni jambo la hakika kwamba ukianza kutumia Twitter au mitandao jamii mingine,utajifunza mambo kadhaa na bila shaka utafurahia. Kama unapenda kusikia “umbea” au udaku utaukuta katika Twitter.Kama unapenda kujua mambo kadhaa kuhusu maendeleo ya ulimwengu wa mtandao,habari za papo kwa papo(breaking news),habari za masoko ya hisa,nk.Yote hayo unaweza kuyapata kwa haraka sana kupitia mtandao wa Twitter.


Sababu Ya Nne: Kama una wasiwasi au uoga kwamba mtandao wa Twitter pengine ni mgumu sana kuuzoea au kuutumia,naomba nikuhakikishie kwamba ni rahisi sana kuutumia.Lugha inayotumika,ujuzi au ufundi wa kuingia na kutoka,kutuma vitu,nk ni jambo rahisi sana kulielewa.Ukishaanza tu kuutumia,utaona jinsi wengine wanavyofanya na utaelewa ilivyo rahisi.Kwa hiyo ni rahisi kuutumia,shaka ondoa.

Sababu Ya Tano: Baadhi ya watu wamewahi kuniambia kwamba wanahofia kutumia mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter kwa kuhofia usalama wa habari zao au kupunguza uwezo wako wa kufikiri(zimewahi kutolewa hoja za namna hiyo kwa wanaopinga matumizi ya Twitter na mitandao jamii mingine).Kama ilivyo rahisi katika kujiunga ni rahisi pia kujiunga bila kujulikana na kila mtu(labda wewe mwenyewe na watu wako wa karibu sana) na pia ni rahisi kujitoa.Usalama upo.Habari kwamba Twitter wanachofanya ni kuisaidia serikali ya Marekani katika kukusanya taarifa za watu,nchi nk hazina msingi wala utafiti wa hakika wa kiinteligencia.

Sababu Ya Sita: Twitter na mitandao mingine ya kijamii sio sehemu tu ya “wateja” au “walevi” wa masuala ya mitandao au jamii, ni sehemu ya watu wote wanaopenda kujifunza jambo moja au jingine kutoka kwa watu au kubadilishana maarifa. Kwa mfano,mojawapo ya mambo ambayo mimi binafsi nayafurahia sana katika utumiaji wangu wa mtandao wa Twitter ni pamoja na kusoma au kupata habari.Kwa sababu takribani vyombo vyote vya habari duniani vinazo akaunt zao maalumu za Twitter,basi upatikanaji wa habari zote muhimu kupitia mtandao huo ni rahisi. Utasoma na kujifunza mengi kutoka kwa watu,vyombo vya habari nk.Jiunge na Twitter leo. Bonyeza hapa kufanya hivyo.

Je,kama wewe unayesoma habari hii tayari unatumia mtandao wa Twitter,nini maoni yako kuhusu Twitter.Unakubaliana na sababu hizo hapo juu?Unazo za nyongeza au za kupunguza? Account yako ya Twitter ni ipi ili “tukufuate”?

Imeandikwa na 

Jeff Msangi ambaye ni Mhariri Mkuu na Mmiliki wa Mtandao wa Bongo Celebrity.Unaweza kuwasiliana naye kupitia jeffmsangi at bongocelebrity.com au jeffmsangi at gmail dot com. Katika Twitter unaweza kutufuata kwa Akaunti @BongoCelebrity

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. none sence.tutachotwa akili na wamarekani hadi lini jamani?..,kifupi siipendi mitandao ya kijamii kama nn sijui..kama vile nisivyoipenda blackberry...

    ReplyDelete
  2. what a bunch of bollocks, kweli we akili ndogo kweli ndugu yangu huo wote uloandika hapo upuuzi hauna maana yeyote wakina lady gaga wanapewa hela ku tweet ok its business like anyother business wewe haikusaidii lolote zaidi ya kupoteza muda mitandao ya jamii inaongoza kwa kupoteza mida na haman kingine

    ReplyDelete
  3. nimeshindwa kama nicheke au nisikitike baada ya kusoma hii makala.kichwa cha habari na maelezo havifanani. halafu mwandishi an mawazo ya kitumwa ya kudhani kuwa kila kitu akifanya mzungu ni kizuri na kina faida.mwandishi pia anasema ukitaka kujua maendeleo ya ulimwengu uende kwenye account ya twitter. kweli wewe ni mwandishi wa celebrity wa ki bongo.

    ReplyDelete
  4. umeshindwa kuni-convince kabisa! lete sababu nyengine, na kwanza ondoa sababu numbari moja haraka.

    ReplyDelete
  5. Me nashauri watu kabla hawajatuma makala zao kwa Ankal kwanza watafute ushauri japo kwa wake/waume zao kabla yakutuma.
    Hii itasaidia kupunguza utumbo na ubabaishaji hapa jamvini.Pia itamsaidia Ankal kupunguza wingi wa makala zisizo na msingi.
    Ni ushauri tu.

    ReplyDelete
  6. Hivi kama ni mtihani unategemea maksi ngapi?

    ReplyDelete
  7. Jamaa ametoa ushauri tu sioni sababu ya kuwa negative naye. Na watoa maoni wengine wala hawaeleweki ni vigeu geu, kwa mfano no.#1 amesema haipendi mitandao ya kijamii lakini yumo humu kwenye blog la Mithupu anatoa maoni. Je huu sio mtandao wa kijamii? Wengine wanasema tutatekwa kimawazo na Wamarekani.Nawaomba muache kuongea pumba, kwani mpaka sasa unatumia mtandao ni Wamarekani ndio waliogundua, mnajua ila buishi tu, kubali matokeo. Mwenzetu akileta wazo siyo lazima kila kitu upinge tu, pima vizuri kwanza. Tuache chuki binafsi.

    ReplyDelete
  8. Mtoa mada katumwa na FBI.
    hii mitandao ya kijamii inatumiwa ili kukusanya data zenu, gharama imekua nafuu sana kwa CIA na wapuuzi wote!
    Angalieni video chini, nini alisema mkurugenzi wa CIA kuhusu facebook

    http://www.youtube.com/watch?v=xAq6QFt8sXU&feature=share

    ReplyDelete
  9. Hizi habari zenu zote zinaandikwa vitabu, waafrika mnavyofikiria n.k. twitter, skype, michuziblog ni data zinaingia katika mashini za jeshi la marekani na zinajichuja wenyewe na kuandika vitu huko, mkigombana chadema na ccm zinajichuja wenyewe. Kwa nini unapenda au kupinga twitter, baadae utakuta data imetengenezwa, ambayo ni taarifa kubwa kwa wenzetu, sisi tunaona upuuzi. Sisi tumeshaliwa basi tubaki kuuwana wenyewe kwa wenyewe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...