Mtangazaji mkongwe Sekione Kitojo wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani (DW)  akiwa na wachezaji wa timu  ya daraja  la  kwanza nchini Ujerumani , Bundesliga, FC Augsburg, Juu akiwa na  Koo kutoka Korea ya kusini na chini akiwa Marcel Ndjeng mwenye asili  ya Cameroon na ambaye pia  ni mchezaji wa timu ya  taifa  ya Cameroon, alipotembelea hivi karibuni mjini Augsburg kwa vekesheni.  Kitojo anakumbukwa na wengi kama mmoja wa watangazaji hodari wa mpira enzi za Radio Tanzania Dar es salaam, enzi za kina Charles Hilary, Salim Mbonde, Ahmed Jongo na  wengineo.
Picha na mdau Malumbo Salim jr.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Sekione Kitojo namkumbuka sana kwenye mpira enzi wa Radio TZ. Picha ya kwanza ametokea kijana mno hadi nilidhani ni mtoto wake.

    ReplyDelete
  2. Ni kweli..Sekione Kitojo enzi za RTD ulikuwa unatangaza mpira vizuri sana..sauti yako ilikuwa bomba mkuu.Nilikuwa bado mdogo,nilidhani umeshakuwa mzee..bado unadai!!

    David V

    ReplyDelete
  3. Angekuwa Tz angeshachoka na maisha, lakini Ulaya bado ni kijana.

    Hapa Tz angeishia na pombe kwa wiiiingi (oh samahani wadau!) ukizingatia kwamba chakula chenyewe michosho basi ungemkuta yuko hoi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...