Abiria 35 na wafanyakazi wane wa ndege ya shirika la Ndege Tanzania (ATC) wamenusurika katika ajali ya ndege (pichani juu) iliyotokea asubuhi ya leo majira ya saa 4.15 katika uwanja wa ndege wa Kigoma.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SSP Kihenya Kihenya amesema aina ya ndege ni Dash 8 Q 300 air tannia flight No. TC 119 iliyokuwa na abiria thelathinin na tano na staff wanne
Alisema ndege hiyo ilikuwa inatoka Kigoma kwenda Dar es salaam kupitia Tabora kabla ya kupata ajali baada ya kuteleza na kuangukia ubavu wa kulia kutokana na tope jingi lililokuwepo katika njia ya kurukia ya uwanja huo.
Abiria na wafanyakazi wote waliokuwamo waliweza kutoka katika ndege salama muda mchache baada ya jaribio lake la kupaa angani liliposhindikana.
Baadhi ya abiria waliohojiwa baada ya ajali wamewasifia sana rubani Emmanuel Mshana na msaidizi wake Mbwali Masesa kwa kujitahidi kuidhibiti kiuweledi ndege hiyo na kuokoa maisha ya watu.
Uchunguzi wa awali unaonesha bawa la kulia pamoja na injini ya propela ya upande huo vimeharibika vibaya.
Mmoja wa abiria walionusurika akiongea na wanahabari
| Kaimu Kamnda wa Polisi mkoa wa Kigoma SSP Kihenya Kihenya (kulia) akiwa eneo la tukiio na maafisa wengine. Picha na Pardon Mbwate wa Jeshi la Polisi |




Laa haula wala kuwwata! Mwenyezi Mungu ni mkubwa.
ReplyDeletePoleni sana kwa matatizo na hongereni sana kwa kusalimika na ajali ya ndege.
poleni sana mlionusurika katika ajali hiyo na pia msisahau kumwomba na kumnshukuru MUNGU siku zote.
ReplyDeleteswali langu ni je hao marubani pamoja na wahusika wengine wote hawakuona kua hali ya uwanja sio nzuri kwa ndege kupaa au kutua??
mnaposema ajali imesababishwa na kuteleza kwa ndege kutokana na tope jingi katika njia ya kupaa inaonesha basi kulikua na uzembe to underestimate the situatuion before taking off.
tuwe waangalifu zaidi
Poleni sana, lazima mumshukuru Mungu. M/Mungu akupeni maisha marefu na yenye amani na furaha.
ReplyDeleteMi nafikiri Tanzania tusiruhusiwe kumiliki ndege hadi tutakapokuwa tayari vya kutosha. Nyie wazungu, msituuzie ndege, sisi bado wajima...eti matope uwanja wa ndege!
ReplyDeleteKama hiyo ndege itakuwa haifai kutengenezwa, gharama ya kuweka lami ni nafuu kuliko hiyo ndege
ReplyDeleteNA HATUNA NDEGE NYINGINE....ILIKUWA HII TU
ReplyDeleteDAVID V
Yaani hata Lori la kusafisha lami Airport Hakuna?
ReplyDeleteLakini Malori ya kurusha maji ya kuwasha yapo kila kona!
Ngombe wa masikini hazai akiza.............
ReplyDeleteTumshukuru Mungu kwa kuwaepusha na sintofahau. Masikini Tanzania!!! Ama kweli ng'ombe wa masikini hazai.
ReplyDelete