Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Africa Century 4 Development (CC) Fred Simon akizungumza na waandishi wa habari pamoja na kuwakaribisha wakulima wa kilimo cha kisasa kutoka makampuni 13 ya nchini Afrika Kusini ambao wamekuja Tanzania kwa ajili ya matembezi ya kujifunza mbinu mbali mbali za kilimo na kuangalia fulsa za kuikwamu Tanzania katika mpango wa kilimo kwanza.
Katibu Mtendaji wa Tanzania Youth Agriculture Foundation (TYAF) Bw. Gasper Mahekula akitoa maelezo machache ya taasisi yao mbele ya wakulima kutoka nchini Afrika Kusini pamoja na waandishi wa habari ambapo aliwakaribisha wageni hao kuwekeza katika kilimo.
Mkutano wa waandishi wa habari pamoja wakulima wa kilimo cha kisasa kutoka Afrika Kusini.
Wageni wakifuatilia mkutano huo.
Wa kwanza kulia ni Mtaalam wa Mambo ya Utawala wa Kilimo wa Kampuni ya IIQ ya Afrika Kusini Bw. Ockie Olivier ambaye ameongozana na wenzake wakifuatilia mkutano huo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Konsortium, Afrika Kusini Bw. Braam Coetnee (kushoto) akiwa na mmoja ya wenyeji wao (katikati) pamoja na Kiongozi anayehusika na mambo ya nje ya Kampuni ya Konsortium, Afrika Kusini Bw. John Luscombe jijini Dar es Salaam.


Halhala wasijetuletea ya Zimbwabwe, manake tungeshughulikia kuwakuza wakulima wetu kabla ya kuleta wageni. sioni mwisho mzuri wa sera hii ya kilimo kwanza
ReplyDeleteKUMBE MDAU TUKO PAMOJA WATATULETEAJE WATU WA NJE? MBONA ZAMANI CHAKULA KILIKUWA KINATOSHA? AU NDO 10% MAKE WATANZANIA HATUCHELEWI
ReplyDeleteJAMANI TUSIUZE NCHI YETU KWA MAKABURU
Jamani huu ni uwenda wazimu kabisa. Watanufaika makaburu na wajanja wachache wa kitanzania. A very bad idea. Kaburu matata! Hawa watu hawajabadilika kichwani wala moyoni. Ila watanzania kuwakumbatia bila kufikiria. Hatujasoma ya Mbarali yaliyoandikwa kwenye Raia Mwema? A very bad idea. Tutalia kilio cha kusaga meno! Ifutiliwe mbali hii tabia ya kuwakumbatia tu hawa watu wabaguzi. Tujenge chetu sisi wenyewe. Tanzania haina wajomba jamani tujitegemee!
ReplyDeleteThe Boers look most unimpressed by whatever has been presented to them by their Tanzanian hosts. The body language does not augur well. Tatizo la watanzania kuangalia mambo juu juu tu! Kaburu bado hajasamehe mswahili kutwaa madaraka kule bondeni na watanzania hamjui bado maana ya kisasi mpaka mtakaogutuka Kaburu anawafanyia nini. Kisasi cha Kaburu kinaendelea kimykimya hata hivi ninavyoandika. tanzanite si yenu tena, benki kubwa iliyokuwa yenu si yenu wameichukua tena kwa bei ya chini mno, Mwalimu wenu mpendwa hamnaye tena na bado.... sasa na ardhi yenu mtawapa. Wake up guys msidanagnyike na lawalawa na visoda. Mnauza nchi.
ReplyDelete