Mwanzilishi mwenza wa Jamii Forums Maxence Melo
Kila mara, katika muongo au muda fulani,huibuka kitu ambacho kwa namna moja au nyingine,hugusa wengi na kuwa na msukumo fulani.Bila shaka tunakubaliana kwamba katika masuala ya shughuli za watanzania mtandaoni,mtandao wa Jamii Forums,unaweza kukidhi haja ya nilichokisema;kugusa wengi na kuwa na msukumo.
Yapo mengi ya kujifunza pale Jamii Forums.Lakini Jamii Forums ni nini,walianzia wapi,nini malengo?Uhuru wa mipaka ya kujadili na kujadiliana unazingatiwa kwa namna gani?Maswali ni mengi.Hivi karibuni blog yetu dada ya BongoCelebrity ilimtafuta mwanzilishi mwenza wa mtandao huo,Maxence Melo, na kufanya naye mahojiano.
Maxence Melo na mwenzake wamefanikiwa kuanzisha ukumbi uliojaa uchochezi wa chuki, majungu na udini. Nashangaa Ankal umempa fursa amwage sumu yake ya miiba hapa kwenye blogspot (yaani issamichuzi.blogspot.com) ya umoja na upendo kati ya Watanzania wa makabila, rangi na dini zooooote!
ReplyDeleteBro Michuzi nadhani ni Jamii Forum (singular) na si Forums (plural) kama unaongea kuhusu ile forum ya slaa, mbowe na kyademaolgy (ha ha ha).
ReplyDeleteAnkal naomba umwabie huyo mwanzilishi au sijui nani,
ReplyDeleteJF wanachochea sana machafuko ya damu na CHUKI baina ya dini, wanatukana sana hasa dini ya kiislamu, ni kubeza , matusi na kutoheshimu kabisa imani ya dini ya kiislam,
Zikija hoja kuhusu Zanzibar kwa kuwa waislmu utaona wanaosemwa sio wazanzibar bali ni dini na imani ya kiislamu,
Naomba unifikishie ujumbe huu WAAMBIA HAO WAKUBWA WA JF KUWA WANAENEZA CHUKI BAINA YA WATANZANIA ambao wamekaa kwa amani kwa muda mrefu sana, wao ni kioo cha jamii kama ni kweli kwanini waruhusu vitu kama vya imani ya dini vijadiliwe? kweli inafaa ifungiwe hii kama itaendelea hivo. Juzi juzi kulikuwa na matusi ya nguoni ya kumtukana Mtume Muhammad na mke wake bibi Aisha kweli niliskitishwa sana kusoma habari ile! JF INACHOCHEA MAPIGANO YA IMANI ZA DINI ! waambieni waache mara moja mijadala inayovunja amani kwa misingi ya imani za dini
Ahsante Ankal
HONGERA SANA M. MELO KWANI JF IS THE LEADING BLOG IN TANZANIA YAANI KILA SIKU LAZIMA NIINGIE.
ReplyDeleteJF ni kiboko jamen. Mimi pale MMU nimetia timu. Sioni kwa nini watu watoke povu wakati kama hupendi siasa kama mimi unatembelea forum inayokuvutia. I real admire you the founder! Natembelea jukwaa la siasa tu pale ambapo kuna issue imetokea Tz kwani najua ntapata information toka kwa source si magezeti na TV zinazochakachua. Mmenifanya nijue mengi kuhusu nchi yangu japo niko mbali kwa sasa. Pongezi saaana
ReplyDeletehttp://youtu.be/xuaBQwuAbYE
ReplyDelete