Na Mwandishi wa Jeshi la Polisi Zanzibar

JESHI la Polisi Zanzibar limepiga marufuku maandamano na mihadhara ya aina yoyote visiwani hapa hadi hapo itakapotangazwa tena.

Taarifa ya Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina, imesema kuwa hatua hiyo inatokana na agizo la Serikali la kusitisha shughuli zote za mikusanyiko ya vikundi vya kidini vikiwemo vile vyenye usajili na ambavyo havina ili kuepusha uvunjifu wa amani.

Akisisitiza msimamo huo wa Jeshi la Polisi, Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Mussa Ali Mussa, amesema Jeshi la Polisi litachukua hatua kali kwa mtu ama kikundi chochote kitakachokaidi agizo hilo kwa lengo la kudumisha amani na usalamawa viisiwa hivyo.

Kamishna Mussa amesema Jeshi la Polisi limelazimika kutoa msisitizo huo kufuatia taarifa za viongozi wa kikundi cha Uamsho kuwatangazia wananchi kuwa kesho wangefanya mhadhara kwenye viwanja vya Lumumba kinyume na maagizo ya Serikali.

Amewataka Wananchi wakiwemo waumini wa dini zote kutojitokeza kushiriki mhadhara huo na mihadhara mingine itakayotangazwa katika kipindi hiki cha marufuku ya mikusanyiko ya aina hiyo.

Jana akizungumza na Waandishi wa Habari mjini Zanzibar, Kiongozi wa Kikundi cha Uamsho Sheikhe Farid Hadi, alisema wangefanya mhadhara mkubwa hiyo kesho jioni na kufanya maandamano Jumanne ya Juni 26, mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 04, 2012

    wametishia muhadhara usifanyike lakini umefanyika watu tumeshachoshwa ndo maana tunaingia mitaani na tuonekana wanuni potela kwa mbali, mhadhara ulifanyika tena kwa amani kubwa sana tuna mshukuru Allah kwa hilo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...