Bendi ya African Stars “Twanga Pepeta” kuanzia tarehe 1 July 2012 itakuwa ikitoa burudani katika ukumbi wa Mzalendo Pub uliopo maeneo ya Makumbusho katika jengo la Millenium Tower.
Burudani itakuwa ikitolewa ukumbini hapo kwa kila siku za Jumapili mara baada ya kumalizika kwa Bonanza linalofanyika kila siku za Jumapili mchana kuanzia saa nane mpaka saa mbili za Usiku.
Twanga Pepeta wameamua kutoa burudani ukumbini hapo mara baada ya kuitikia maombi ya muda mrefu kutoka kwa wapenzi wa Twanga Pepeta wanaoishi maeneo ya jirani na Mzalendo Pub.
Sisi watanzania sio wabunifu,huo mtindo wa unenguaji tangu ulipoletwa na wazaire haubadiliki,hivi mnajua kuwa watu wamekinai huo mtindo jaribuni kuiga mwingine basi au mpaka DRC waletendo tuige????? aibu kwani kuwa msanii lazima uwe mbunifu na sio muigaji.
ReplyDeleteHalafu mbona wanavaa mavazi tofauti sana, inapendeza wakivaa style za nguo zinazofanana kidogo, sio mwingine suruali , na mwingine kaptula etc
ReplyDelete