Mkurugenzi Mtendaji wa MKUKI NA NYOTA PUBLISHERS Bw. Walter Bugoya akitoa neno wakati wa uzinduzi wa kitabu cha 'FURAHA HUJA ASUBUHI' (JOY COMES IN THE MORNING) kilichoandikwa na Hopolang Phororo kinachozungumzia Mateso na manyanyaso ya wasichana wadogo wakati wa malezi yao na haki ya msingi ya jinsia ya kike katika jamii.
Mgeni rasmi Mwenyekiti Mtendaji wa TACAIDS Dkt. Fatma Mrisho akitoa nasaha zake wakati uzinduzi rasmi wa kitabu hicho jijini Dar es Salaam. Alisema 66% ya wanawake na 20% ya wanaume nchini wameshawahi kukutwa na majanga ya unyanyasaji wa Kijinsia  katika maelzi yao ambapo kwa sasa Dar es Salaam na Mbeya zinaongoza. 
 Mtunzi wa Kitabu cha 'JOY COMES IN THE MORNING' Bi. Hopolang Phororo akielezea simulizi ya kweli iliyomkuta kama mwathirika wa unyanyasaji wa Kijinsia wakati wa usichana wake na moyo, uvumilivu aliokuwa nao wa kuweka uzoefu huo katika maadishi ili jamii ijifunze na madhara ya unyanyasaji wa Kijinsia unaokua kwa kasi nchini Tanzania.
Mmoja wa washiriki wa uzinduzi huo  akitoa neno la shukrani wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Hopolang Phororo na haki za msingi za wanawake wanaokutwa na matatizo ya unyanyasaji wa Kijinsia Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 08, 2012

    Ningependa kununua hiki kitabu je ni duka gani la vitabu hapa mjini Dar naweza kukipata.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 08, 2012

    misupu mbona hujatuambiye ni bei gani hichi kitabu kinaonekana ni kizuri sana na wapi kinapatikana

    mdau u.s.a

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...