TAARIFA ILIYOIFIKIA GLOBU YA JAMII HIVI PUNDE,INAELEZA KUWA MELI YA ABIRIA ILIYOTAMBULIKA KWA JINA LA MV. SKAGET ILIYOKUWA IKIELEKEA ZANZIBAR KUTOKEA JIJINI DAR ES SALAAM NA ILIYOKUWA NA ABIRIA ZAIDI YA 200,IMEPINDIKA NA KUANZA KUZAMA BAADA YA KUZIDIWA NA MAWIMBI MAKUBWA YALIYOKUWA YAKIPITA BAHARINI.
AJALI HIYO IMETOKEA MUDA MFUPI ULIOPITA KATIKA KISIWA CHA CHUMBI AMBAPO NI MPAKANI KWA DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR.
VYOMBO VYA UOKOAJI VIKO NJIANI KUELEKEA ENEO LA TUKIO HIVI SASA NA LIBENEKE LA GLOBU YA JAMII LINAENDELEA KUFUATILIA KWA UKARIBU TUKIO HILO NA TUTAENDELEA KUPEANZA TAARIFA KADRI ZINAVYOPATIKANA.
Ooh!yale yale tena ya kuzidisha abiria? Mungu awanusuru wote waokolewe wakiwa salama.
ReplyDeleteTUWAOMBEE HERI NDUGU ZETU.
Ohoo, yale yale!!! http://wolfganghthome.wordpress.com/2012/02/20/zanzibar-news-updae-mv-skagit-stopped-from-sailing-to-pemba-by-zam-over-safety-concerns/
ReplyDeleteEee mwenyezi mungu mwingio wa rehema tuepushe na maafa na wasafiri wote waokolewe watanzania tuungane kwa sala.
ReplyDeleteYA'ARABI TUNUSURU WAJA ZAKO,YA'AALLAH!
ReplyDeleteHIVI NINI!MUNGU WANGU TUOKOE TUMEZIDIWA SASA!!!!
NIMESTUKA MNO JAMANI MIMI!
KUFUNGUA TUU,HII HABARI IKO JUU!!
TUSAIDIANE KUMUOMBA MWENYEZI MUNGU SANA!
ATUKINGE NA HAYA MAJANGA!
AHLAM,,LONDON
huu ni msiba mkubwa kwa mara nyengine tena! hivi vyombo vya usafiri vya majini huwa havizingatii habari za hali ya hewa??? my thoughts and prayers to the families of the deceased, and wishing quick recovery kwa wale walioumia. what a tragedy!
ReplyDeleteHivi Dunia nzima vyombo vya usafiri tunamiliki sisi pekee?
ReplyDeleteHivi ni kwa nini Kanuni,vigezo na mashariti,Taratibu na Sheria ktk uendeshaji wa vyombo na biashara za usafiri havizingatiwi?
Tutakwisha hadi lini?
Wazanzibari tufuate taratibu na kanuni na tusipende vitu kwa njia za mkato na magendo!
Inawezekana Meli haikuwa na vigezo vinavyostahili lakini ikalazimishwa kwa njia za mkato mkato kuendesha biashara.
Je, kwa madhila haya tutapata kulaumiana ya kuwa hizi ndio kero za Muungano?
Tuwaombee wasafiri
ReplyDeletevp ankali mbona kimya hizo taarifa nusu nusu tupashe basi tuhabarike vyema kinaga ubaga.
ReplyDeleteinna lillahi waina illahim rajiun rahman atuwafikishiye salaama ndugu zetu wazazi wetu, jamaa zetu, marafiki zetu na majirani zetu . amin.
ReplyDeletemdau New York
Imepindikaje?Unamaanisha ilikatikakatikati au namna gani,sijaelewakichwa cha habari.
ReplyDelete...innaa lillahi wa innailahi rajiun!jamaan eeh,enyi wadau wa vyombo vya usafiri vya majini 2seme ume2pangia ki2 gan haswa?kutumaliza au?timizen wajibu wenu kwanza maslah baadae!msiufanye usafir wa majin kuwa usafiri hatarishi!
ReplyDelete