Mwaka 1948 Sinodi ya Kanisa ilimwomba Pd. Van Melssen kutafuta eneo sehemu za undali bila mafanikio. Mwaka 1949 eneo dogo lilipatikana mjini Tukuyu karibu na ofisi za ustawi wa jamii. Mwaka huo huo Pd. Melssen alipeleka ombi kwa uongozi wa Wilaya kuomba eneo kwenye barabara iendayo Igale umbali wa 25 Km kutoka Tukuyu Mjini. Aliomba kati ya eka 30 hadi 40. na alisema eneo hili lingekuwa zuri kwa ajili ya kulima kahawa. Ni mwaka 1952 ndipo Wakatoliki wakafanikiwa kupata eneo Igogwe lakini badala ya eka walizoomba waliambulia eka 4 tu. Pd. Poels alifungua shule ya msingi mwaka 1953, na Pd. Melssen hali akijua pingamizi kubwa la kuanzisha kilimo cha kahawa alipanda miti 1000 ya kahawa.

Baraza la Maaskofu la mwaka 1956 liliamua kujenga misioni mpya baada ya ile ya Ipinda iliyojengwa miaka 20 iliyopita. Jimbo lilikuwa na eneo Igogwe lakini Baraza halikutaka kujenga eneo hilo kwa vile ingeweza kuhudumiwa vema na Parokia ya Kisa. Waliona vema kuanzisha maeneo ya Mwakaleli. Mapadre: Van Melssen, Hoppe na Poels walienda Mwakaleli kuomba kupata eneo kutoka kwa uongozi wa mahali pale kupitia kwa mkuu wa Wilaya bila mafanikio.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...