Baadhi ya wadau wa masuala ya blog nchini wakiwa katika picha ya pamoja jioni hii katika hafla fupi iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania kuwatunukia tuzo maalum, zoezi ambalo limeahirishwa kutokana na ajali ya meli iliyotokea mapema leo visiwani Zanzibar. Msemaji wa Vodacom amesema imebidi waahirishe zoezi hili ili kuungana na Watanzania wote katika kuomboleza msiba huu mkubwa kwa taifa na kwamba kampuni hiyo ya simu itajiunga katika juhudi zozote za kujitolea kwa hali na mali katika maombolezo na kuwafariji waliopatwa na maafa pamoja na wafiwa. Taswira za chini ni za wadau hao baada ya kupata habari za ajali hiyo.



Haki Ngowi na Matina Nkurlu na wadau

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 19, 2012

    well done VODACOM, mumejifunza sana. Ilipozama Spice Islanders muliendelea na sherehe bila ya kujali janga lililotokea. Huu ndio Uungwana, sote ni ndugu na ni wateja wenu.
    Mdau, Zenj

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 19, 2012

    mithupu hiyo fish eye yako tutakoma mwaka huuu

    ReplyDelete
  3. Hawa mabloga walichaguliwa lini na kwa kigezo kipi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...