SEMENI BASIL KAVISHE
(25 MACHI 1975 – 11 JULAI 2011)
Dada Mpendwa SEMENI BASIL KAVISHE ( Mama Sophia), leo ni tarehe 11/7/2012 imetimia mwaka mmoja toka ututoke duniani.
Hatupo nawe kimwili lakini kiroho upo nasi, tunakumbuka kwa upendo wako, hekima na busara zako.
Daima unakumbukwa na mumewako mpendwa Nasoro Manzi Salim, mwanao Habiba Nasoro, baba yako, wadogo zako, wajomba zako, mama zako wadogo na wakubwa, shemeji zako, wifi zako na wanafamilia wote wa Basil Kavishe, Yakub Lisomba na Manzi Salim.
Mwenyezi Mungu akulaze mahala pema peponi Amina.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...