1. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na mgeni wake Rais Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia alipowasili Ikulu jijini Dar es salaam  kwa maongezi rasmi pamoja na dhifa ya kitaifa.
  2. Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiwa na mgeni wao Rais Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia alipowasili Ikulu jijini Dar es salaam leo kwa maongezi rasmi pamoja na dhifa ya kitaifa.Hapa akisalimiana na Baadhi ya wanachunzi waliofika Ikulu kumlaki mgeni huyo. PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 18, 2012

    Mapokezi mazuri sana, hakika ni heshima kwa nchi yetu

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 18, 2012

    KAKA MICHUZI HIVI KUMBE BENDERA YA LIBERIA INAFANANA NA YA MAREKANI??NAOMBA KUJULISHWA TAFADHALI

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 18, 2012

    Liberia ilikuwa moja ya state za marekani inasemekani hao wa Liberia ni baadhi wa watumwa waliorudishwa kutoka marekani na kupewa makazi hapo sina uhakika sana. anayejua atujuze pls

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 18, 2012

    Hawakurudishwa, bali kuna baadhi wa watumwa wenye asili ya Africa walikimbia utumwa huko marekani na walipotua na meli zao, wakafikia pwani ya Africa mashariki ndio ambayo ikaja kuwa nchi ya libelia, wakanzisha na serikali na utawala wao na bendela kila kitu, na jamii nyingine ya kiafrica kwa wakati huo walikuwepo eneo hilo , wengi wao walikua wanaishi mapolini mbali na pwani, na hao waliotoka marekani wakajita Americo, na kama unavyona bendela kama sehemu mmoja ya wamarekani

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 18, 2012

    Hongera! Hongera! Rais Kikwete pamoja na First Lady kum karibisha Rais wa Liberia. Wakati wa Kinamama sasa! Kwa Rais Kikwete pamoja na First Lady ni mafunzo makubwa kwa waTanzania kutoka kwa Rais wa Liberia. Kila kheri! Songa mbele Tanzania! Dr. Migiro 2015 iko karibu vipi wakinamama Tanzania? wakati ndiyo huu waku jitarisha! Je Tanzania iko tayari kuongoza na wakinamama!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 18, 2012

    Tafadhali annanymous hapo juu fanya mapitio ya yale unayoandika kabla ya kutuma. Watumwa hao walifikia pwani ya Afrika ya Magharibi na siyo pwani ya Afrika ya Mashariki. Kuhusu bendera ya Liberia ina nyota moja tu tofauti na ile ya USA ambayo ina nyota nyingi kila moja ikiwakilisha jimbo (state)

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 18, 2012

    Ulishaona nchi zilizoendelea kuwa na mapokezi ya watu kibao wamejipanga barabarani? Tena wanafunzi. Shule kwishne kwa siku hiyo na kama kazi hakuna/hakuna uzalishaji. Tutazidi kuwa maskini milele.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 18, 2012

    He siku hizi Liberia iko pwani ya Afrika Mashariki? Mkiambiwa msikimbie somo la Jiografia hamsikii!! Haya tena lete story na Tanzania iko pwani ya Afrika Magharibi lol!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 18, 2012

    Anonymous wa 12:46:00 masahihisho kidogo

    Hawakukimbia utumwa bali walikuwa ni watu weusi ambao waliweza kununua uhuru wao au walioweza kutunukiwa uhuru wao kutokana na vigezo fulani enzi hizo(wengi wao walikuwa mchanganyiko na wazungu-"half caste" au wasomi, au watumwa ambao walifanya kazi kwa wadhifu na kusababisha wamiliki wao wawaachie). Kutokana na kunyanyasika japokuwa walikuwa huru yaani wazungu bado waliwatenda kama vile watumwa kwa sababu ya rangi yao nyeusi ingawa walihesabika kuwa huru. Hawakuweza kumiliki ardhi, kupata kazi kama watu weupe na walithibitiwa katika mambo mengi. Kwa msaada wa Serikali ya Marekani, watu weusi hao wakashauriwa kurudi barani Afrika na kuanza maisha kama wakoloni katika nchi ya Liberia. Wakakabidhiwa silaha na fedha na kukwea kwenye meli mpaka Liberia. Kufika Liberia sasa, wao ndio wakawa kama watawala. Na wao wakaanza kuwanyanyasa waafrika ambao waliowakuta huko. Wakaipindua serikali na kuwa wamiliki wapya waliberia. Tokea hapo siasa ya Liberia ikawa ndio ya kupinduana tu na mavita kila siku kwa sababu waafrika asilia na watu weusi wahamiaji kutoka marekani walikuwa hawaelewani (na sababu zingine). Kwa hiyo Liberia ina bendera kama Marekani kwasababu ilikuwa koloni la Wamarekani (weusi na huru enzi za utumwa)barani Afrika.

    Wanahistoria mbalimbali wanadhani kwamba hio ilikuwa ni njia tu ya kuwafukuza watu weusi hao kwa sababu uhuru wao ungesababisha watumwa wengine wagome au kwa kuwa hawakuwahitaji tena.

    Dada J.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 19, 2012

    Halloo!!! Nasahisha hapo juu, sio Pwani ya Africa mashariki, ni magharibi, nilipitiwa wadau

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 19, 2012

    Mhe. Raisi JK nimegee kidogo na mimi !

    ...umbea unanisumbua...

    Je, kicheko chako picha ya chini kimeletwa na nini?

    Nahisi Madame Ellen Johnson Sirleaf Raisi wa Liberia amevutiwa na Wanafunzi wa kike akakwambia ni wakati wao sasa wewe JK ukitoka Ofisini uwape na wao!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...