Spika wa Bunge la Afrika ya Mashariki, Magreti Nzziwa Nantongo (kulia), akibadilishana mawazo na Mbunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania, Shy Rose Bhanji. 
 Wabunge wa Afrika Mashariki Shy Rose Bhanji na mwenzake kutoka burundi wakibadilishana mawazo na spika wa bunge la Afrika ya Mashariki, Magreth Nzziwa (katikati), kutoka Uganda ambaye ni spika wa kwanza mwanamke toka kuanzishwa tena EAC.hapa wakiwa kwenye kikao cha kupanga kazi za mwaka za bunge hilo katika Hotel ya East Afrikan jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 12, 2012

    Mheshimiwa Shyrose,

    kwanza hongera sana kwa kuchaguliwa kutuwakilisha katika Bunge la Afrika Mashariki.

    Mbali ya Kushinda Uchaguzi, Jamani Mtuwakilishe vizuri, someni sana current International Affairs, muelewe Dunia inakwenda wapi?

    Mjuwe National Interests zetu Kama Tanzania ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ni zipi, na mzisimamie na kuzipigania kwa nguvu zote.

    Msione aibu kuomba ushauri, Tanzania ina Hazina kubwa wa watu wenye Uzoefu wa mambo mbali mbali lakini wanaweza wasiwe wabunge kama nyinyi.

    Kikubwa Zaidi, Jaribuni kila wakati kuongea kwa Sauti Moja kama Taifa *Tanzania* kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizopo na sera za Serikali yetu zinazohusiana na Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki.

    Kila la Kheri

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...