Habari wadau, naomba kuwajulisha kuwa nimepata taarifa kwamba mwandishi mwenzetu Criss Mwambonda amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.

Taarifa kutoka kwa ndugu yake aitwaye Obi pamoja na rafiki yake wa karibu Jimmy Chika ni kwamba taratibu za mazishi zinafanywa nyumbani kwao Mbezi, Dar es Salaam.

Mambo mengine kuhusiana na jambo hili tutajulishana wadau. Ni msiba wa wote na sote njia yetu ni moja.

Tumuombee Mwenyezi Mungu amuweke mahala pema peponi, marehemu Mwambonda ambaye amefanya kazi vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini.

Ahsanteni.

Amir Mhando
Katibu Mkuu - TASWA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...