Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Wilbald Lorri  (pichani) kuwa Msaidizi wa Rais, Masuala ya Lishe (Nutrition).

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano, Julai 18, 2012 na Ofisi ya Katibu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue, kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inasema kuwa uteuzi huo wa Dkt. Lorri ulianza tokea Juni Mosi, 2012.

Kabla ya uteuzi wake, Dkt. Lorri ambaye ana shahada ya uzamivu (PhD) katika Sayansi ya Lishe alikuwa mtaalam wa lishe katika Mradi wa Feed the Future unaoendeshwa nchini na Shirika la Maendeleo la Marekani - USAID.

Aidha, kati ya mwaka 1994 na 2003, Dkt Lorri alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula na Lishe Tanzania – (Tanzania Food and Nutrition Centre).

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
18 Julai, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 19, 2012

    The guy needs to diet.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 19, 2012

    Hahaha mkuu wa Nutrition lakini ukiangalai afya mmmhh... Ila wadau sijaelewa hii nafasi yaani ni mshauri wa diet ya Raisi au Lishe ipi? Natanguliza shukrani.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 19, 2012

    Aisee!!! Mungu ni mwema,naamini utafanya yale uliyokuwa ukiyafanya lishe, nimeamini mungu kweli akitaka lake linakuwa, waliofanya majungu, fitina na umbea wako wapi kina ndossy sasa, aibu kwao! Keep it up Baba.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 19, 2012

    Lishe kwa vitendo!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 19, 2012

    Hujakosea kumteua mpambanaji.....mtu wa watu kisha mpiga kazi! Dr. Lorry kapige kazi nakuaminia kaka!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 19, 2012

    nimefurahishwa sana na uteuzi wa huyu mbaba, ni mchapakazi sana na mpenda haki ila walimpiga majungu mengi sana alipokuwa tfnc, ila ndio hivyo sasa kauchinja....

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 19, 2012

    Hongera sana Dr Lorri umetufanyia kazi nzuri sana feed the future ubarikiwe tunaamini utaendelea kuwa mpambanaji wetu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...