Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Servacius Likwelile akichangia mada kuhusu nini kifanyike ili kuimarisha Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa katika ngazi ya Kitaifa. Katika Mchango wake, Bw. Likwelile amesisitiza kwamba ili Ofisi ya Mratibu Mkazi iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu inatakiwa ijengewe uwezo kwa kuongezewa wataalamu, fedha na vifaa. Amesema kwamba kutokana na Tanzania kuwa moja kati ya nchi Tisa ambazo zimejitolea kushiriki utekelezaji wa Mpango wa Ufanyaji Kazi wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa ( Delivering as One) imebaini kwamba kunaumuhimu wa kuiimarisha ofisi hiyo ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu yake na uwajibikaji lakini pia kupunguza urasimu na ukiritimba ambapo kila jambo linatakiwa kutolewa maamuzi kutoka Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Baadhi ya Maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Tume ya Mipango wakifuatilia majadiliano yalivyokuwa yakiendelea, majadiliano ambayo pia yalihusisha mjadala kuhusu uboreshaji wa Ofisi ya Mratibu Mkazi ambapo Tanzania kupitia Naibu Katibu Mkuu, Servacius Likwelile licha ya kuelezea umuhimu na faida za Delivering as One hususani kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania, alisisitiza kuwa licha ya kwamba kumekuwapo na mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mpango huo, lakini imebaini kwamba bado kuna kazi ya kufanya ikiwamo hiyo ya kuimarisha na kuboresha utendaji kazi wa Ofisi ya Mratibu Mkazi wa UM katika ngani ya Kitaifa. Aliyekaa mbele ni Bw. Jerome Buretta kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Pastory Masomhe kutoka Tume ya Mipango, Bw. Jimreeves Naftal kutoka Wizara ya Fedha wakiwa na aliyewahi kuwa Mratibu Mkazi wa UN nchini Tanzania, Bw. John Hendra ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu Msaidizi na Naibu Mkurugenzi wa sera na mipango katika Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Masuala ya Wanawake ( UN-WOMEN).


Na huyo aliyeinamisha kichwa chini ni nani?? Well done Mr. Likwelile.
ReplyDeleteAlieinamisha kichwa chini AnaChat Good Job Mr. Likwelile
ReplyDelete