TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
         
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bibi Winfrida Beatrice Korosso kuwa Katibu wa Tume ya Kurekebisha Sheria nchini.

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano, Agosti 22, 2012 mjini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inasema kuwa uteuzi huo ulianza Agosti 14, mwaka huu, 2012.

Kabla ya uteuzi wake, Bibi Korosso alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mkurugenzi wa Mashtaka katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
22 Agosti, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. hongea bi dada chapa kazi.

    ReplyDelete
  2. Hongera sana Dada Winnie. Mwe nhobwike fijo. Congratulation Nndenga mafumu gahobwike.

    ReplyDelete
  3. ALL THE BEST DA WINNIE YOU DESERVE IT.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...