Mgombea nafasi ya Uewenyekiti Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT),Halima Mohamed Mamuya akirudisha fomu ya kuomba kugombea nafasi hiyo kwa Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni UWT Makao Makuu Riziki Kingwande jijini Dar es salaam jana.Mamuya aliyekuwa Katibu Mkuu wa zamani wa umoja huo, anakuwa mtu wa tatu kujitokeza kuwania kiti cha uenyekiti wa UWT ngazi ya taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Safi sana mamaa chukua kiti uimarishe jumuia iliyokufa hiyo.mh rais nae aelewe hao watu wake wanamuangusha sasa ni wakati wa kuimarisha chama.ccm oyeeee

    ReplyDelete
  2. Hongera Halima, naamini unaweza, unajiamini, unastahili na pia uhakika upo wa kushinda na kuinyakuwa nafasi hiyo ya uwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT). Nakuombea kila la kheri ufanikiwe INSHA ALLAH.

    ReplyDelete
  3. I support you Halima Mamuya. Tulikuwa wote Ruvu na Mbweni JKT.

    ReplyDelete
  4. Jamani hivi kila mtu anamjua huyo Mamuya? Maana habari hata haisemi ni yupi kati ya hao wawili!

    ReplyDelete
  5. Mdau wa maguAugust 06, 2012

    Huyo halima ndio yupi katika hyo picha? nani anamkabidhi form mwenzie katika hiyo picha?

    ReplyDelete
  6. Mimi Halima simjui lakini picha inaonyesha kuwa ni wa Kushoto,,Maana chekaji ya wa kulia,inaonyesha yeye mwenyeji hapo,na tabasamu la wa kushoto linaonyesha kaleta hiyo fomu..
    Kwa upande mwingine naweza kusema Halima ni wa Kulia maana inaonyesha kisha kabidhi fomu kisha anataka kutoa mkono kwa mpokeaji fomu,vile vile wa kulia inaonekana yuko kweli ofisini kwake.
    Inatatanisha sana,,Ingekuwa majina ya dini tofauti tungejuwa nani kajistiri Ramadhani!

    Ahlam...London

    ReplyDelete
  7. Mamuya mi naona huyo alievaa magamba

    ReplyDelete
  8. Hongera sana Da-Halima. Ila hatutarajii kina mama mnaogombea nafasi hiyo ya uongozi kutukanana kama watoto, tafadhali sana epukeni kutupiana matusi na kashfa. Uchaguzi uliopita ilikuwa aibu tupu, malumbano, kashfa na matusi ya kila aina kutoka kwa watu wazima na waliokuwa wanaheshimika katika jamii, kisa????? uenyekiti wa UWT. Chonde, chonde jamani, msitudhalilishe wanawake wenzenu. Mkubali na kuelewa kuwa asiyekubali kushindwa si mshindani. All the best big girls!!!

    ReplyDelete
  9. Halima ni huyo mwenye nguo zenye rangi ya chama chetu.

    ReplyDelete
  10. Halima ni huyo mwenye mawani na amevaa kitenge cha KIjani, mtandio wa njano. Kwa mliosema hamumjui Halima ni yupi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...