Mchezaji wa Pool wa Klabu ya Jambo Lee, Michael Saita akicheza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya Mkoa kwa awamu ya pili katika klabu ya Jambo Lee Kawe jijini Dar es Salaam.Kulia ni mchezaji wa klabu hiyo Judith Machafuko.

Na Mwandishi Wetu

MASHINDANO ya Safari Pool Taifa yamefunguliwa tena jana kwa awamu ya pili baada ya kusimama kwa mwezi mmoja kwa mfungo wa Ramadhani.

Akizungumza na waandishi wa habari Mhazini wa Chama cha Pool Taifa, Zaholo Ligalu alisemakatika awamu ya kwanza mikoa kumi tayari imeshakamilisha mashindano hayo ya ngazi ya mikoa na mikoa sita ndio inakwenda kuanza leo kumalizia awamu ya pili baada ya mfungo wa Ramadhani ambayo ni Mbeya,Iringa,Dodoma, Temeke,Ilala na Kinondoni.

Ligalu alisema Kinondoni,Temeke na Ilala wanaanza leo ambapo Mbeya ,Iringa na Dodoma wataanza Septemba 6 mwaka huu na kumaliza Septemba 9 mwaka huu.

Alisema Ligalu mashindano ya mwaka huu yanahusisha timu za vilabu kwa ngazi ya mikoa na fainali za kitaifa ambazo zinatarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 27,28,29 na 30 mwaka huu ambapo klabu ambayo ni bingwa wa mkoa ndio atawakilisha Mkoa katika mashindano hayo

Zawadi ya mshindi wa kwanza kwa ngazi ya Mkoa upande wa timu ni shilingi laki saba na kwa ngazi ya Taifa itakayofanyika mkoani Mwanza mshindi atajinyakulia kitita cha shilingi milioni tano

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...