Habari zimetufikia punde kwamba magari matatu yameshika moto Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar usiku huu. Inasemekana moto ulianzia kwenye gari moja aina ya  Range Rover kabla ya kusambaa kwenye magari ya aina ya Toyota na Corolla kabla ya kuzimwa na zimamoto waliofika hapo muda mfupi baadaye. Habari zaidi baadaye....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Vipi michuzi Mbona Hamna habari za binti aliyebakwa hadharani vingunguti kwa kuvaa uchi? Naona ni kitu wasomaji wako wangehitaji kujua kabisa

    ReplyDelete
  2. Haya Magari Freelander / Range Rover yote Jamii ya landrover sijui yana laana Gani? Any way Nina kama matukio Matatu nimeshughudia haya aina ya Magari yakiungua Moto!!

    ReplyDelete
  3. Kwani corolla si Toyota ?

    ReplyDelete
  4. Hizi Range za kununua kwa dili ndio tatizo lake. Poleni wahusika wote.

    ReplyDelete
  5. Pole kwa waathirika wote. Tukio hilo lingetokea mbali na Uwanja wa ndege sipati picha madhara yangekuwaje.

    ReplyDelete
  6. Mdau wa kwanza hiyo habari ya binti kubakwa si kazi ya MICHUZI peke yake maana si kwamba kila tukio analijua. Wewe kama ulikua unaifahamu ulitakiwa umtumie na ametoa contact zake for any BREAKING NEWS hivyo ni jukumu lako pia kumtumia ili yeye afanye verification ya hizo information

    Mdau Igwamanoni wa Itabagumba

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...