Mkufunzi wa masuala ya aundaaji wa Filamu kutoka taasisis ya Sanaa na uandishi wa Habari (IAMCO) Ngalimecha Ngahyoma, akizungumza jambo katika Jukwaa la Sanaa, kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) Hassan Bumbuli na kushoto ni Katibu Mtendaji wa BASATA Ghonche Materego

Na Mwandishi Wetu

Wasanii wa nchini wametakiwa kujiimarisha katika masuala ya taaaluma ili waweze kufanya kazi zenye ubora na zinazokidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchini.

Akizungumza katika Jukwaa la Sanaa jana, mkufunzi wa masuala ya uandaaji wa filamu hapa nchini Ngalimecha Ngahyoma amesema kumekuwa na matatizo mengi katika uandaaji wa kazi za filamu hapa nchini kutokana na wasanii kutokuelewa misingi ya uandaaji wa filamu.

“Kuna maeneo ya msingi ambayo yanahitaji watu kubobea ili kuyafanya kwa utimilifu, na hakuna njia ya mkato ni lazima kuyapata shuleni kwa maana lazima mtu ufundishwe. Wasanii wengi wanatumia vipaji vyao, lakini matokeo ya kufanya mambo kwa vipaji ndiyo haya ambayo yanatupa filamu zenye matatizo katika maeneo mbalimbali,” alisema.

Alisema ni muhimu kwa wasanii kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kuanza kuandaa kazi kitaalamu ili kufanya kazi zilizobora na kwamba ni vyema kutumia wataalam katika maeneo yote yanayohitaji utalaam badala ya mtu mmoja kufanya kazi zote.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Ghonche Materego, amesema suala la taaluma alikwepeki katika kutengeneza kazi zenye ubora na kuwasisitiza wasanii kujiunga na vyuo kupata utaalam katika fani zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...