Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Dodoma, Antony Mavunde akirejesha fomu za kugombea nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kwa Mkuu wa Idara ya Siasa Oganizesheni ya UVCCM Taifa, Sophia Duma. Zoezi la urejeshaji fomu kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za UVCCM ulitaraji kufikia tamati jana jioni kwa wagombea wote kutakiwa kutejesha fomu zao.
Mdau Innocent Meleck nae ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya Umakamu Mwenyekiti UVCCM waliorejesha fomu za kugombea nafasi hiyo leo kwa Mkuu wa Idara ya Siasa Oganizesheni ya UVCCM Taifa, Sophia Duma.
 Daniel Zenda akirejesha fomu za kugombea nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kwa Mkuu wa Idara ya Siasa Oganizesheni ya UVCCM Taifa, Sophia Duma.
 Lulu Abas Mtemvu nae alirejesha fomu zake za kuwania Ujumbe wa NEC kupitia UVCCM.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Watu wanatafuta ulaji sasa. Tuwe makini kuchagua viongozi imara ambao wapo kwa maslahi ya taifa na sio maslahi yao binafsi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...