Sehemu ya uharibifu uliofanywa na wavamizi hao huko Ugiriki usiku wa kuamkia leo

Habari ankal Asante kwa kuniwekea habari zangu nyingi kuhusu Ugiriki, licha ya baadhi ya watu kuona tunawabania kuja Ugiriki na kuuliza kwa nini nyie mpo kama kuna matatizo Ukweli ni huu Chama cha XRISI AVGI au Golden down(Neo Nazi) kimeanza piga piga ya wageni wakiongozwa na wabunge wao ambao polisi inashindwa kuingilia kati wakiwepo.

Yaani usiku wa kuamkia leo   Septemba 26, 2012  ofisi za Jumuiya ya watanzania ziliharibiwa vibaya na baadhi ya watu kujeruhiwa. Licha ya kuwepo kwa Polisi bado walishindwa kuzuia tukio hilo na kuonekana polisi wakiwapa mgongo kabisa Watanzania baada ya hapo walielekea maeneo mengine ya mabaa ya wageni yaliyopo karibu na kuharibiwa vibaya pia Baadhi tu ya picha na news pia zipo kwenye mitandao mingi tu.

Mdau Umangani

Wadau wkiwa nje ya ofisi za Jumuiya iliyovamiwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Huku si mnaona tunavyochinjwa na vyombo vya Uhasama! Kazeni boot, maisha ni mapambano!

    ReplyDelete
  2. poleni sana wadau ila rudini kwenu jamani.

    hata huku maisha yapo.

    yaani hawa watu millioni 41 hawatoshi kuonesha kua maisha yapo?
    or what else do you want?

    ReplyDelete
  3. Kufeni kidume lakini bongo msirudi mpaka mpate pasi ya kigiriki halafu mtahamia UK.

    ReplyDelete
  4. Ugiriki, Portugal, Italy, Spain, na baadhi ya nchi nyingi za Ulaya uchumi uko kwenye matatizo makubwa sana.

    Nyie wenye mabaa na biashara zingine kwenye nchi hizo lazima mtakuwa mnaonekana mko na 'hali nzuri'.

    Hivyo basi ni lazima watakunyimeni amani maana kibao kimegeuka, cha msingi wekezeni zaidi nyumbani maana sisi huku thamani yetu huwa ni ileile, IKO JUU.

    ReplyDelete
  5. Msikubali kuonewa Mnaweza kuwashitaki kwenye mahakama za kimataifa.
    Mimi nilisha washitaki wangu na nikishinda kesi watanilipa zaidi ya dola 19000.
    Inaudhu sana ninapoona Watanzania wananyanyaswa.
    We subiri tutengeneze nyumbani ili turudi na wao wakija kule na ujinga wao wa unaziz tuwape kipigo kitakatifu.

    ReplyDelete
  6. Poleni sana wenzetu wa Ugiriki, wakati umefika na sisi kuwafanyia hivyo kwa wagiriki waliopo hapa nchini ili nao waone MUZIKI wetu.

    ReplyDelete
  7. Kaka mkiona hivyo hamtakiwi tena la msingi kama si cha sekondari mwaanzage kufungasha!!
    Na huku baado ardhi kubwa ujuzi mlonao toka huko majuu tukiuchanganya na ushamba wetu tutavuka!

    ReplyDelete
  8. MABO YA KUMCHUKIA MGENI SIKU HIZI YAPO KATIKA MATAIFA MBALIMBALI KAMA AFRICA KUSINI, KENYA, UK, HATA TANZANIA YAPO. POLENI KWA USUMBUFU.
    MATATIZO YA KIUCHUMI NA KIJAMII YANAPOTOKEA SEHEMU YOYOTE WAGENI HUBEBESHWA LAWAMA HATA KAMA HAWAHUSIKI

    ReplyDelete
  9. Piga, ua, galagaza, SIONDOKI, tutabanana hivi, hivi, inajaa ndoo ya maji siyo NCHI.

    ReplyDelete
  10. Sasa nyie mko nchi za watu bendera za nini? Nitafurahi sana siku nikisikia vibaraka wa CHADEMA au CCM wakipingwa mkong'oto na uwe wa nguvu. Kama na uchungu na nchi si mrudi? Hata hapa nchini si tunawalaumu wachina, wahindi wa wazungukwenye madini? Mbao yaho yako dunia nzima, hata ukisema ni kwa sababu ni weuzi mbona Afrika ya kusini mambo yale yale?

    ReplyDelete
  11. mimi watu wanaosihi walio nje kurudi bongo nawashangaa. MBONA wao wameng`ang`ania DAR, warudi jijini waliokotokea KAMA KWELI WAO WAZALENDO . Mmewaacha ngugu zenu hawana maji safi, mnapoteza muda online kuwasiliana na walio ugiriki !!

    ReplyDelete
  12. Ninajiuliza Kwanini walivamiwa watanzania tu? Mliwakosea nini? au hapa Tanzania tumefanya nini kuwakasirisha huko kwao?

    ReplyDelete
  13. Sasa mtalijua jiji bora mie niko tz napata ugali wangu na dagaa kuliko kipigo!

    ReplyDelete
  14. Waliovamiwa siyo watanzania tu bali hata watu wa mataifa mengine.

    Mdau wa ugiriki

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...