Na Dkt N. T. Jiwaji
Masuala ya angani ni ya ajabu na ya kumvutia kila mtu kiasi
cha kuamini kila kitakachowekwa mbele yetu kwa kutumia taswira za Mwezi
mkubwa, mkusanyiko wa nyota zinazomeremeta, na magimba ya angani yenye
maumbo ya ajabu na ya kutatanisha, na kadhalika.
Matukio mawili
ya hivi karibuni yanaonesha umaasuma wetu katika kuamini habari yoyote
inayotolewa, ikichanganyika na shauku tunayopata kwa kusikia habari
za maajabu ya angani. Lakini je hayo maajabu kweli yanaweza kutokea?
Je tumejiuliza ukweli wa maelezo tuliyosikia?
Mkanganyiko wa kwanza ulitokea mwezi uliopita tarehe
31 Agosti, ulikuwa unahusu kuwapo Miezi miwili ya rangi ya bluu. Baadhi
ya tovuti katika mtandao, zilionesha Mwezi mpevu uliowekewa rangi ya
bluu. Kwa bahati nzuri, usiku wa tarehe 31 Agosti, hakukuwa na Mwezi
wa rangi ya bluu ila ulionekana Mwezi mpevu mmoja unaong’ara kwa mwanga
mweupe kama unavyo kuwa kawaida.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...