Na Dkt N. T. Jiwaji

Masuala ya angani ni ya ajabu na ya kumvutia kila mtu kiasi cha kuamini kila kitakachowekwa mbele yetu kwa kutumia taswira za Mwezi mkubwa, mkusanyiko wa nyota zinazomeremeta, na magimba ya angani yenye maumbo ya ajabu na ya kutatanisha, na kadhalika.  

Matukio mawili ya hivi karibuni yanaonesha umaasuma wetu katika kuamini habari yoyote inayotolewa, ikichanganyika na shauku tunayopata kwa kusikia habari za maajabu ya angani.  Lakini je hayo maajabu kweli yanaweza kutokea?  Je tumejiuliza ukweli wa maelezo tuliyosikia?

Mkanganyiko wa kwanza ulitokea mwezi uliopita tarehe 31 Agosti, ulikuwa unahusu kuwapo Miezi miwili ya rangi ya bluu. Baadhi ya tovuti katika mtandao, zilionesha Mwezi mpevu uliowekewa rangi ya bluu. Kwa bahati nzuri, usiku wa tarehe 31 Agosti, hakukuwa na Mwezi wa rangi ya bluu ila ulionekana Mwezi mpevu mmoja unaong’ara kwa mwanga mweupe kama unavyo kuwa kawaida.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...