Khadija Mnoga aka KIMOBITEL akiimba wimbo wake mpya "Mgeni" wakati wa utambulisho wake rasmi wa kujiunga na Bendi ya Extra Bongo ndani ya New White House Kimara Korogwe Dar es salaam usiku wa kuamkia leo.
Kimobitel akiimba na Mkurugenzi wa Extra Bongo Ally Choki wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la "Mgeni" ndani ya New White house wakati wa utambulisho wake rasmi.
Comredi Ally Choki aka Mzee wa Farasi
Kimobitel akizikonga nyoyo za mashabiki wake ndani ya Meeda Sinza usiku wa kuamkia leo wakati aliokuwa akitambulishwa rasmi kwa mashabiki wa maeneo ya Sinza na maeneo ya jirani.
Makamanda wa Extra Bongo wakiongozwa na Ally Choki mwenye Tsheti nyeupe mbele, kutoka kushoto ni Banza Stoni, Kimobitel na mwisho kulia ni Rogert Hega aka Katapila wakiimba wimbo mpya wa Hadija Mnoga aka Kimobitel.
Ally Choki Mkurugenzi wa Extra Bongo akiimba kwa furaha wimbo wa "Mgeni" ulotungwa na Khadija Mnoga (Kimobitel). Mwanamuziki Khadija Mnoga (Kimobitel) wiki iliyopita alitambulishwa rasmi kwa waandishi wa Habari kujiunga na Bendi ya Extra Bongo akitokea bendi ya African Stars (Twanga Pepeta) aliyoifanyia kazi kwa miezi kadhaa. Juzi Ijumaa na Jana Jumamosi ndiyo zilikuwa siku rasmi za kutambulishwa kwa mashabiki na wapenzi wa Extra Bongo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...