Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa Daraja la Kigamboni katika hafla iliyofanyika huko Kurasini jijini Dar es Salaam leo mchana.Kushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli na wapili kulia ni mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt.Ramadhani Dau.NSSF itatoa asilimia 60 za ujenzi wa daraja hilo na serikali itatoa asilimia 40
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisisitiza jambo wakati akiongea na Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni uliofanyika huko Kurasini jijini Dar es Salaam leo mchana.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik
Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli akimpa maelezo Raid Dtk.Jakaya Mrisho Kikwete juu ya Ujenzi wa Daraja la Kigamboni wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa Daraja hilo ulofanyika Kurasini jijini Dar ea Salaam leo mchana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. mh raisi wangu Kikwete me naona hawa jamaa kila siku wanakuletea siasa kwenye ujenzi wa hili daraja maana kila siku linaongelewa mara kuwekwa jiwe la msingi mara kuanza kujengwa mara sasa kuzinduliwa wakati hatuoni likijengwa kwa kasi kama ilivyosemwa. Mh raisi nakuomba usikubali tena wakuite kwenye hii ishu ya daraja waambie tu wakuite likikamilika maana nadhani hawajui cheo cha urais kinavyotakiwa kuwa respected...mdau kigamboni future resident

    ReplyDelete
  2. Big up.... Hongera sana serikali na nssf kwa juhudi..... I pray that ujenzi uende bila tatizo.....

    ReplyDelete
  3. Angalizo, ile haya mabarabara na madaraja ya 'Magufuli' isiwe Dar tu, serikali ikumbuke Tanzania ni kubwa na Tanzania yote inahitaji 'mabarabar', 'madaraja', na pia 'Mareli' ya TAZARA na TRL kwenda mikoani pia iboreshwe ili kuchangamsha uchumi na kuunganisha masoko kwa usafiri wa hakika wa kila aina.
    Mdau
    Mwisho wa Reli
    Tanganyika

    ReplyDelete
  4. Barabara Msata-Bagamoyo, Ya Kuelekea Morogoro, Dar kuelekea Bagamoyo na sasa Daraja la Kigamboni. Mungu ibariki Tanzania. Wape afya njema na upeo zaidi wale wote wanaochapa kazi kwa dhati na si kwa chati.

    ReplyDelete
  5. Tungekua na ''MAJEMBE''haya matatu(Magufuli-Miundombinu,Mwakyembe-Usafirishaji na Kagasheki-Maliasili na utalii)kama ishirini hivi Hakyamungu Tungekua mbali isivyoelezeka...Mungu wabariki hawa mawaziri watatu waendelee kuchapa kazi sio hao wanaoendekeza propaganda za kisiasa tu na utendaji ziro.

    ReplyDelete
  6. Wewe unaemsifia magufuli jembe, JEMBE HAPA NI KIKWETE NA DR DAU, huyo magufuli wenu mbona aligoma daraja lisijengwe ? leo anasifiwa magufuli ! mbona mnamsahau Dr Dau!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...