Kichwa cha treni pamoja na mabehewa sita ya awamu ya kwanza,yakisubiri kufanyiwa majaribio kwa Safari zitazoanzia Station ya Dar es Salaam Mpaka Ubungo mnamo mwezi wa kumi. Majaribia hayo yameongozwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi,Mhe. Dk Charles Tizeba(Mb) ambaye alipanda treni hiyo kuanzia Station Dar es Salaam Mpaka Ubungo.Serikali imetumia kiasi cha Sh. Bil 4.75 kwa ajili ya ukarabati wa njia,injini na mabehewa.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi,Dk. Charles Tizeba(Mb),akipanda treni wakati wa majaribio ya Mabehewa sita ya treni kati ya mabehewa kumi na mbili yanatogemewa kutumika na Shirika la reli Tanzania(TRL). Treni hizo zitakayofanya safari zake kutoka Station Dar es Salaam mpaka Ubungo,mapema mwezi wa Kumi.
Baadhi ya wananchi wakipanda katika behewa moja kati ya Sita yaliyofanyiwa majaribio mapema leo kutokea Station mpaka Ubungo(km 12).
Mchuma huo unaondoka
Baadhi ya Wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania(TRL) wakiwa na furaha ndani ya mojawapo ya mabehewa yaliyofanyiwa majaribio leo abubuhi.
Abiria wa majaribio


Ni vema kuthubutu kuliko kusema haiwezekani. Naamini hili litawezekana, na hata kama litakwama credits zinabaki palepale. Kazi nzuri (endapo tu haikugeuzwa mradi wa mfukoni)!
ReplyDeletemhhh my country,, so sad
ReplyDeleteLakini pamoja na yote kweli hata kusafisha hicho kituo cha kuanzia na kuweka standard imekuwa shida? kweli mtaanza safari hizo kwa hali hiyo na taka zote hizo hapo chini? Kwanini usafi usizingatiwe? Hata mkifungua kuwe na heshima na watu wajue ni kitu cha kuheshimika siyo vurumai tu....!!
ReplyDeleteNyie pondeni tu, mlikimbilia kule kuliko pikwa tayari, na mkakaa kula tu,nyamafu nyie.Lakini punde skin head wakiwabagua tu, tayari kilio -o mimi kwetu sikuua ,kama ndo hivi ,nitarudi kwetu,mara o,africa kuzuri bwana hakunyanyasi mtu.Nyie hao hao o kuchafu !!! sasa tuwaelewe je ??? cheki viti vya treni vilivyotulia ,kabla havijaanza kuchorwa chorwa au kuchanwa na viwembe.Kweli ,wakati mwingine sisi ni choo ile babu kubwa.Lakini, iko dalili ya kuuona mwezi.Zebedayo msema kweli
ReplyDeleteHaya ndio maendeleo
ReplyDeletehiyo biashara ingeachiwa private sector. Kwaattitudes za Wabongo dhidi ya vitu vya serikali, watauwa hiyo biashara mda si mrefu.
ReplyDeleteTukiacha ushabiki serikali inabidi ipongezwe kwa hili na we need to take this as a way forward toward electric-train..but usimamizi uwe makini na endelevu usiishie kwa mwakyembe tu..
ReplyDeleteKuhusu uchafu tusimlaumu mtu kwasababu sisi watanzania ndio wachafu.
ReplyDeleteNashauri wangefikiria kuweka viti cichache ili kupata roooms za ajili ya kubeba abiria wengi.Ingawa mimi ndo 'Geneous' Mwakyembe na wenzake ningeshauri waweke viti vya kuangaliana ili katikati wasimame watu wengi zaidi.Pili katika Dar masterplan reli ilitakiwa iiishie Wazo Hill.nadhani ni wakati muafaka ili lifikiriwe bila kujalai kama kuna watu wamejenga ndani ya njia ya reli
ReplyDeleteBig up Zebedayo msemakweli
ReplyDeleteSasa kituo chenyewe kichafu hakina mpangilio watu wanapanda kiholela madirisha ukiwacha wazi upepo ukifunga ni kama upo ndani ya contena la mizigo
ReplyDeletehivi walishindwa kuweka madirisha ya vioo?
Nina imani huo sio mtaji wa mtu binafsi kama ilivyo kituo cha mabasi ubungo
jengeni vituo vizuri na vidumishwe kwa usafi
Dar Metro, oyeee!!
ReplyDeleteyaani namuunga mkono mdau aliesema hiyo biasha iachiwe private sector kabisaa ndo itadumu alafu jamani hayo madirisha ya treni na joto la dar Mungu wangu mpka ufike ubungo kazi ipo.. Hongera sana serikali ya J.k hapo kweli mmethubutu nadhani mtaweze pia..
ReplyDeleteJamani BREKI.. BREKI zimo???
ReplyDeleteTusije kurudi tena kwenye maafa ya kitaifa yasiyoisha kila siku...oh!!
Ninyi mnaoponda ni wakati wenu sasa kurekebisha !
ReplyDelete1.Wa Majuu mnaotucheka na kukebehi jitihada zetu ni wakati wenu sasa mchangie kinachowezekana ili hali iwe bora zaidi!
2.Mliopo hapa Tanzania, ni wakati wenu sasa angalau hata msipofanya usafi kwa vitendo mchangie mawazo!
3.Sisi tumeanza ninyi mmalizie, sio kulaumu na kudharau!
Hongera!
ReplyDeleteBongo tambarale hali ndio hiyo inaanza kuimarika dege linaanza kuruka!
Wa Majuu tunafanya maandalizi ili mje kupanda Matreni yetu huku Bongo Tambarale mliojengewa na Mababu zenu badala ya kupanda matreni kwa manyanyaso ugenini.
Tunajua wengi meshazoea maisha ya Matreni mmelemaa sasa tunawaandalia usafiri Jijini mkifika mtapewa Vitambulisho mtumie ninyi sisi tutaendelea na usafiri wa Mabasi na foleni za barabara msizoweza ninyi!
Hamjui walilipia kodi mababu zao wakajenga?
Heee Dar-Ubungo?
ReplyDeleteSio Ubungo-Posta?
Kwani Ubungo ni nje ya Dar?
USAFI!!!
ReplyDeleteSehemu za kujisaidia pande zote mbili yaani stesheni kuu na ubungo, VYOO vipewe kipaumbele cha USAFI.
Sivyo vitageuka mazalio ya magonjwa yanayotokana na uchafu.
MAPATO!!!
Mdau wa kwanza kagusia. Pamulikwe tochi hapo ili pajiendeshe itakavyowezekana. Yaani tuwabane wahusika hizo hela zieleweke.
Wabongo sijui tkoje! viti hivyo vitachanwa na treni kuchorwa na makerpen muda si mrefu, sembuse mali ya serikali lol! Haya kila la heri isiishie majaribio.
ReplyDeletehawa wanaoponda shughuli hii wana maslahi yao binafsi kuhusu usafiri wa daaladala hapo Dar. Unajua kuna watu huwa hawapendi mafanikio ya kiujumla ya maendeleo ya raia. Kwa hiyo hao wanaoponda wanajua kuwa watapoteza mapato kutokana na huduma hiyo ya treni
ReplyDeleteWa Majuu mnadai hamtaki kurudi Bongo kwa kuwa huko mliko kuna usafiri wa Matreni.
ReplyDeleteMatreni ndio haya tumewaandalia karibuni nyumbani Tanzania mje mshiriki ujenzi wa nchi!.
Haya sasa kila kitu chini ya jamvi ndani ya Bongo,,,mpo hapo?
Hongera sana!
ReplyDeleteWanaobeza wajinyonge!
Walau,
1.Tumethubutu,
2.Tumediriki,
3.Tumeweza,
4.Na tunasonga mbele!
Je Bandugu tuache unafiki na dharau, hivi miongo kadhaa iliyopita tuliyaona haya?
Mnabeza nini Watanzania?
ReplyDeleteMnaobeza acheni dharau kabisa hapa!
Tazameni mabehewa mazuri tu, viti vizuri makava ya ngozi n.k
Mnachotakiwa mnaobeza ni kutoa mchango wenu badala ya kuwa 'domo wazi' mchango wa jinsi hali hiiitakavyo lindwa ili ubora udumu na hali iimarike zaidi!
Mnabeza nini Watanzania?
ReplyDeleteMnaobeza acheni dharau kabisa hapa!
Tazameni mabehewa mazuri tu, viti vizuri makava ya ngozi n.k
Mnachotakiwa mnaobeza ni kutoa mchango wenu badala ya kuwa 'domo wazi' mchango wa jinsi hali hiiitakavyo lindwa ili ubora udumu na hali iimarike zaidi!
Wewe unaodai chini pachafu kama umeona unangoja nini?
ReplyDeleteSi ungedamka alfajiri na fagio lako hadi Stesheni ya Treni ukafanye usafi?
Wewe unafikiri nchi inajengwa na nani kama sio wewe Mwananchi?
Unafikiri atakuja Mkazi wa Kigali nchini Rwanda aje akufagilie wewe?
Kule Wananchi wanafagia kwa ridhaa yao wenyewe kama mchango wa Ujenzi wa Taifa, kalaga baho!
Tauche tabia ya 'NAFSI LAWWAMMA' tuwe na mwenendo wa 'NAFSI MUTUMAINA' angalieni wajinga wanavyo toa kejeli.
ReplyDeleteKama hizi ni jitihada za kuleta hali bora nchini kwa nyie wakazi wa Gongo la Mboto na Mbezi-Kimara ambao mlikuwa mnawacheka wa Mbagala kwa kupandia madirishani kwenye mabasi na ninyi sasa mnapanda hivyo hivyo!
Sasa mnataka iweje?
Nyie mnaotoa dharau ndio wapanda mabasi madirishani wakazi wa Mbagala, Gongo la Mboto na Mbezi-Kimara!
ReplyDeleteBora watoe hao wa Mbagala reli haipiti kwao sasa nyie wa Mbezi-Kimara na Gongo la mboto si ndio msaada huo?
Nauli ni sh ngapi jamani? nimeipenda .big up.TRl .mwakyembu juuuuuu.
ReplyDeleteMiunda
ReplyDeleteMi namshauri waziri husika afavye anavyo weza kuweza kuondoa uwoza huo wa matrein mabovu.
Kama upo wezekano afanye anavyoweza atafute wawekezaji,usafiri huu waachiwe watu binafsi au mashika binafsi ili wauendeleze,watafute mtu kama mwenye company ya Virgen,aje tuunganishie mikio yote kwa train za kisasa.
itasaidia kukuza uchumi kwa haraka pia baadhi ya mikoa kufua masoko ya biashara kwa usafiri wa uhakika na wa haraka.
Mdau Miunda.
ni muda muafaka tuanze kupongeza pale jambo zuri linapofanyika na tutoe mawazo ya namna ya kuboresha. hii ni njia sahihi katika kupunguza msongamano wa magari na pia kupunguza udhia wa usafiri kwa hiyo njia. sasa changamoto ni namna ya kufanya lidumu na kukidhi jukumu lilopo
ReplyDeleteHongera kwa Mwakembe...
ReplyDeleteMchaka chaka uendelee...
tunataraji mengi kutoka kwako.
Mlikuwa wapi nyakati zote hizi? Fanya Udhubutu, Reli ipandishe hadi Wazo Hill. Compensations zimetafunwa miaka mingi kupisha extension ya reli kutoka ubungo. Ila kwa Ufisadi wetu!!!!Kazi kweli kweli
ReplyDelete@ zebedayo.
ReplyDeleteThe thing is uchafu unaonekana hapo, walio nje ya nchi ofcourse ni lazima waseme, kwani hata kufanya usafi tanzania inahitaji mwekezaji? ni vyanzo vya magonjwa hivyo! system ndio mbaya , that's it.
Hapa DSM kuna makabila 300 wengine wametoka vijijini hata vyoo hawakuacha huko, kaenda sekondari, wanajisaidia vichakani kaingia chuo kikuu cga DSM kusoma kile choo pale College of Arts harufu yake wale hawaisikii wanaona ni kitu cha kawaida kwa sababu kujisaidia katika bidet anaona tusi kwake. Sasa takataka za barabarani yeye akaweke wapi. Hujaona barabara ya Morogoro mzungu anajenga na kusafisha asubuhi ili kesho aweke udongo mzuri anakuta magunia ya taka yamelundikwa katikati pale KAGERA. Watanzania ni wachafu, huko katika mahekalu yanayoshamiri kila siku ukiende usiombe kwenda chooni. Utamaduni wa kutunza choo hana mtu. Usimwone kavaa tai.
ReplyDelete