Umoja wa Watanzania Ujerumani (UTU)  Unapenda kuwakaribisha  wanachama wote wa UTU, Katika Mkutano mkuu wa UTU. Utakaofanyika Katika ukumbi Uliopo Ringstr. 109, 65479 Raunheim).  Siku ya Tarehe 29.09.2012, Kuanzia saa 08:00 Mchana. Tunawaomba wanachama wote  wa UTU mhudhurie katika mkutano huu muhimu. Na kwa wale ambao sio wanachaama na wanahitaji kujiunga na UTU, tuandikie barua pepe kamati.utu@googlemail.com au unaweza kuwasiliana na Mwenyekiti kupitia simu ya mkononi. 0173-4298997 Karibuni sana.
Ili uweze kupiga au kupigiwa kura inabidi uwe umelipia ada ya Kiingilio cha uwanachama, na uwe umelipa  ada ya uwanachama wa mwaka mzima.
Bank Informations
Union of Tanzania in German e.V
Acc. No.59641
BLZ 71160161
VR BANK Rosenheim-Chiemsee eG
 MALAZI:
Malazi yatapatikana Hotel Attachè Raunheim) http://www.attache.de/de
Angalia details zote ta hoteli hii kwenye attachment niliyoambatanisha. Hoteli iko karibu na Ukumbi wa Mkutano, ni karibu dakika 10 hivi kwa mguu.
Address ni: Hotel Attachè, Frankfurterstr. 34, 65479 Raunheim Tel: 06142-2040, e-Mail: welcome@attache.de

Uzuri ni kuwa bei hii nafuu tumepewa sisi Watanzania kwa ajili ya Kikao hiki, kwa hivyo kila atakayefanya booking lazima ajitambulishe kwa kutumia (TANZANIA ORGANISATION - cc. Dr. Majura)  Ningependekeza mbali na kufanya booking moja kwa moja, ingefaa pia wamjulishe Bw. Majura kuwa wamefanya booking ili tuwe na orodha kamili.
kiwa watakuwepo watu wengi wa kutosha, basi tutapewa Hotel nzima kama ifutavyo:

8-    Single Bedroom    (Watu 8)           -   Euro 50,- kila chumba
11- Double Bedrooms (Watu 22)        -   Euro 50,- kila chumba
4-   Three Bedrooms    (Watu 12)        -   Euro 65,. kila chumba
4-   Small Double Bedrooms (Watu8) -  Euro 50,- kila chumba 
Break First ni Extra
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Hi did i just read Break First instead of Break Fast?

    ReplyDelete
  2. Ughaibuni watu wana-share chumba ama kweli hali ngumu!!

    ReplyDelete
  3. Angalau ughaibuni watu wana-share chumba, bongo watu wanashare kitanda, timu kubwa kama yanga inawaweka wanaume wawili walale kitanda kimoja, mtu anaweza kupatwa na jinamizi akaanza kuota ndoto za kifirauni.

    ReplyDelete
  4. Masuala ya kushare ndio mwanzo wa maradhi kama ya Mfadhaiko!

    Matokeo yake badala ya watu kuamka asubuhi na kuanza Kikao Frankfurt-Ujerumani watu wanaanzia Kituo cha Polisi kutoa maelezo ya Mashitaka!!!

    ReplyDelete
  5. Mdau wa Nne (4),

    Hahahahaha

    Kwa Ulaya hapo kwenda Polisi kutoa maelezo asubuhi?,,,enhhh kule hapo hapo tukio linajiri ukibonyeza button wana wa Makunjas ndani ya nyumba!

    Nchi zingine kama Marekani ukipiga simu yeyote 911 Wazee bila maelekezo wanakuja inaonyesha moja kwa moja kuwa ni wapi kuna shida!

    Utadhani Polisi za wenzetu ni Mashetani au Majini?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...